Waziri Mkuu azindua mpango wa ugawaji wa mbolea bure kwa wakulima 83,000 nchini
Balozi
wa Norway Nchini Bi.Elisabeth Jocobsen(wapili kulia) akizunguma jambo
na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa(wapili kushoto) mara baada ya kuzindua
mpango wa kusambaza mbolea bure kwa wakulima
wadogo nchini mpango umeratibiwa
na Kampuni ya YARA Tanzania kupitia mradi wa uitwao Action Africa ambapo zaidi ya tani 12,500 zitatolewa. kushoto
ni Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga
na Kulia ni Mkurugenzi wa YARA Tanzania Winstone Odhiambo.
Waziri Mkuu Kassim
Majaliwa akizungumza jambo katika uzinduzi wa rasmi wa ugawaji wa mbolea bure kwa
wakulima zaidi ya 83,000 nchini uliofanyika ofisi za kampuni ya YARA Tanzania jijini Dar es Salaam
na kumeratibiwa na Kampuni hiyo
kupitia mradi wa Action Africa ambapo zaidi ya tani 12,500 zitatolewa.
“Nachukua fursa hii kuipongeza kampuni ya YARA kwa kujitoa kwake kuchangia kwenye kukuza sekta ya kilimo kwa kutoa mbolea bure kwa wakulima zaidi 83,000,” alisema Waziri Mkuu Majaliwa.
Alisema ni muhimu watenda wa serikali wakashirikiana na kampuni ya YARA kutimiza lengo la kuwafikishia mbolea wakulima kwa wakati na bure kama ilivyopangwa.
“Watendaji wasiwe kikwazo katika utekelezaji wa mpango huu ambao unalengo la kuwanufaisha hasa wakulima wadogo ili kuongeza uzalishaji wa mazao nchini.
Aidha, ametoa wito kwa makamuni mengine yanayojihusisha na sekta ya kilimo kuiga mfano huu wa YARA kuboresha sekta kwa kuondoa changamoto zinazowakabili wakulima.
“Natumia nafasi kuyataka kampuni mengine kujitoa ili kusaidia sekta hususani kwenye swala la pembejeo na zana za kilimo kwa kuwa kilimo ni sekta inayoajiri zaidi ya asilimia 75 ya watanzania,” alisema Majaliwa
Kwa upande wake Waziri wa Kilimo Bw.Japhet Hasunga alisema wizara yake pamoja na mamlaka za uthibiti zimejiridhisha kuwa mbolea ya YARA inafaa kwa matumizi kulingana na mazingira ya nchi yalivyo na hivyo itachochea kuongeza uzalishaji wa mazao ya mahindi na mpunga.
“Taratibu za kufanya ithibati ya mbolea hii zimezingatiwa hivyo tunaimani zitachangia katika kuongeza ubira na uzalishaji wa mazao nchini,” alisema Hasunga
Alisema Serikali itaendelea kwa kuhamasisha na kuhakikisha wakulima wanapata elimu ya matumizi ya mbolea na mbegu bora na viua tirifu zinavyofaa kulingana na ardhi yetu ili kuongeza uzalishaji ili nchi ijitosheleze kwa chakula.
“Serikali imejipanga kuhakikisha masoko ya mazao yanapatikana ili mkulima aweze kufaidika na shughuli yake jambo litakalo chochea ukuaji wa uchumi na maendeleo kwa ujumla,” alisema Hasunga
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya YARA Tanzania,Bw.Winstone Odhiambo alisema mpango huu ni jitihada za kampuni mama kutoka Norway kuhakikisha nchi za Afrika ikiwemo Tanzania zinajitosheleza kuzalisha chakula.
“Mpango huu wa usambazaji mbolea bure unafanyika kupitia mradi maalum ujulikano kama ‘Action Africa’, “ alisema Odhiambo na kuwataka wakulima hapa nchini kuchangamkia fursa hiyo kugawiwa mbolea bure.
Aina za Mbolea zinazosambazwa na kampuni ya YARA Tanzania ni NPK ambapo zaidi ya MT 12,500 zitatolewa kwa wakulima wadogo kote nchini kwa kujisajili kupitia namba *149*46*16#.
Comments
Post a Comment