Viongozi wa ushirika Rukwa wapata mafunzo kutumia matrekta kuinua kilimo

 
Kaimu Meneja Mkuu wa Kampuni ya Agricom Africa inayojihusika na usamabazaji na uuzaji wa zana za kilimo,Bw.Remmy Nindi akizungumza katika uzinduzi wa Programu ya matumizi ya zana bora za kilimo mkoani Rukwa iliyolenga kuwajengea uwezo wakulima katika kutumia zana hizo ili ziwaletee mafanikio katika shughuli za kilimo.


Mkuu wa Ufundi wa Kampuni ya Agricom Africa,Bw.Philipo William akitoa maelekezo ya matumizi ya moja ya zana za kilimo viongozi wa vyama vya ushirika mkoani Rukwa ikiwa ni sehemu ya uzinduzi wa Programu ya matumizi ya zana bora za kilimo  Mkoani humo yaliyolenga kuwajengea uwezo wakulima katika kuzitumia zana hizo ili ziwaletee mafanikio katika kilimo.

Na Moses Ferdinand, Sumbawanga 
Viongozi wa ushirika Mkoani Rukwa wanapata mafunzo ili vyama vya msingi vya ushirika viweze kusimamia kwa ufanisi matumizi ya matrekta  kama ilivyoainishwa katika mpango wa kuinua sekta ya kilimo awamu ya pili (ASDPII).

Mafunzo hayo yanatolewa  kabla ya Kampuni ya  Agricom  Africa Company Limited kutoa matrekta kwa vyama vya msingi vya ushirika ili kuinua uzalishaji wa mahindi katika kila wilaya ya mkoa wa Mpanda. Kwa mujibu wa programu hii chama cha msingi chenye wananchama wanaozidi 72 ambacho kitakuwa na fedha ya awali ya kulipia matrekta kitapewa matrekta ili kuinua uzalishaji wa mazao na kuinua kipato cha wakulima kama ASDP II inavyotaka.

Akizindua mafunzo hayo hapa jana Katibu Tawala Msaidiz (Uchumi na Uzalishaji) Bw.Ocram Chengula, ameisifu  kampuni ya Agricom Africa  kwamba  inatekeleza kwa vitendo programu ya  ASDP II. “ASDP II imejielekeza katika kuhakikisha matumizi ya zana bora za kilimo zinawafikia wakulima nchini ili kuongeza tija ya uzalishaji mazao nchini.  Kampuni hii ASDP II kwa vitendo,” amesema Bw.Chengula

Amesema asilimia kubwa ya wakulima wa Rukwa wanatumia jembe, wanyama kazi na wachache wanatumia matrekta  na kuongeza kwamba mafunzo hayo yatakuwa chachu ya kuanza kutumia zana za kisasa katika na kuinua kilimo biashara, na kuongeza kwamba uzinduzi wa programu hiyo utaongeza hamasa ya uzalishaji wa mazao hususani mahindi nakuufanya  mkoa  kutosheleze kwa chakula  na iuzwe na kuinua kipato cha wakulima.

Mkoa wa Rukwa una hecta  574,291 nzuri za kilimo ambazo kwa kiasi kikubwa zinamilikiwa na wanachama wa vyama vya msingi vya ushiriaka.   Kwa kawaida hekta 303,393 kila mwaka hupandwa mazao ya nafaka na mboga.  Kati ya hizi hekta 1,049 ( au asilimia 0.3) hupandwa mazao wakati wa vuli na hekta 302,345 (aslimia 99.7) hupandwa mazao wakati wa masika.

Kaimu Meneja Mkuu wa Kampuni ya Agricom Africa, Bw. Remmy Nindi, amesema kampuni yake inaelewa mkoa wa Rukwa una  fursa kubwa za uzalishaji wa mazao ya mahindi.  

“Rukwa ina nafasi kubwa ya kuzalishaji kwa wingi zao la mahindi kutokana na ardhi yake. Hivyo kwa kuwapatia elimu ya matumizi ya zana za kisasa za kilimo kutaongeza uzalishaji mara tatu ya walivyokuwa wakizalisha awali,” amesema Bw.Nindi. Amesema kampuni yao ina matawi Morogoro,Mbeya,Dodoma na Kahama.

 Mrajisi Msaidizi wa Vyama vya Ushirika, Bw.Benjamin Mangwala, ofisi yake itahakikisha matumizi sahihi ya zana za kilimo zitakazo milikiwa na vyama vya msingi vya ushirika ili kuwaletea  maendeleo wanachama wa vyama hivyo.

“Tutaandaa mwongozo wa namna bora ya kusimamia matumizi ya zana hizi katika vyama vya ushirika ili wanachama wake waweze kunufaika na pia iwe sehemu ya kuwaongezea kipato katika vyama kwa kutumia zana hizo katika shughuli mbalimbali,” amesema Bw.Mangwala



Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa Pwani asifu juhudi za mmiliki wa Makampuni ya Global Packaging na Wande Printing

17 projects to house 80,000 tonnes of crops being built

Tanesco: Azma ya uchumi wa kati na wa viwanda ifikapo 2025 inatekelezeka