TNBC kufanyia kazi mapendekezo ya wataalam kuhusu mazingira ya biashara
| Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la
Biashara(TNBC) Dkt.Godwill Wanga (katikati),akizungumza jambo na waandishi wa habari kwenye hafla ya
uzinduzi wa repoti ya mazingira ya Kibiashara
kwa makampuni ya Nordic nchini
Tanzania na kuahidi kuwa watakwenda kufanyia kazi changamoto zote
zilizojitokeza ili kuchochea uwekezaji na biashara
nchini. kulia ni Katibu Mtendaji
wa Taasisi ya Utafiti wa Sera na Maendeleo(REPOA) Dkt.Donald Mmari na kushoto ni Balozi wa Sweden Nchini
Tanzania Bw.Anders Sjoberg.
|
Na Abdallah Luambano, Dar es Salaam
BARAZA la Taifa la Biashara (TNBC) limepokea ripoti iliyoandaliwa na Taasisi ya Utafiti ya REPOA kwa kushirikiana na nchi za Sweden,Denmark, Norway na Finland inayoeleza hali ya uwekezaji na mazingira ya biashara kwa nchi hizo hapa nchini na kuahidi kuyafanyia kazi mapendekezo yaliyomo.
Akizungumza katika hafla ya makabidhiano ya ripoti hiyo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam, Katibu Mtendaji wa wa TNBC, Dkt Godwill Wanga alisema kuwa tafiti zenye weledi zinazoelezea hali ya mazingira ya biashara na uwekezaji zinachagia kwa kiasi kikubwa katika kutatua changamoto zilizopo na kuweka mazingira mazuri zaidi ya kibiashara.
“Leo tumepokea ripoti kutoka REPOA ambayo inaeleza namna serikali ilivyofanikiwa kuweka mazingira rafiki na kuwezesha biashara na uwekezaji pamoja na kutaja maeneo ambayo bado changamoto,’’ alisema Dkt. Wanga na kuongeza kuwa serikali imedharia kuhakikisha kuwa mazingira ya biashara yanaendelea kuimarika na kuvutia wawekezaji zaidi.
Dkt. Wanga alisema kuwa licha ya jitihada kubwa zilizochukuliwa na serikali katika kuweka mazingira rafiki ya ufanyaji biashara Tanzania, zipo baadhi changamoto ambazo serikali kupitia Baraza zinaendelea kuzifanyia kazi.
“Kumekuwepo na jitihada kubwa za serikali katika kuweka mazingira rafiki ya biashara ikiwemo punguzo la tozo mbalimbali pamoja na ushirikiano wa serikali na sekta binafsi.Pamoja na hayo yote mazuri changamoto hazikosekani hivyo kupitia baraza zitaendelea kutatuliwa ,’’ alieleza.
Ameahidi kuwa serikali itafanyia kazi ripoti hiyo kwa kupata majibu ya chagamoto zilizopo hasa kwenye upande wa kodi, uhamiaji hasa upatikanaji wa vibali vya kufanya kazi hapa Tanzania, ubora wa bidhaa pamoja na utaalam.
Kwa Upande wake Balozi wa Sweden nchini Tanzania Balozi Anders Sjoberg alisema, licha ya changamoto zilizopo wataendelea kuita wawekezaji kuja kuwekeza Tanzania kwa kuwa mazingira yanayojengwa sasa ni mazuri lakini sababu nyingine ni mahusiano mazuri kihistoria baina ya nchi hizo.
“Mazingira ya biashara Tanzania ni mazuri licha ya changamoto zilizopo, tunaamini watu wetu wataendelea kuja kuwekeza na kufanya biashara kwa kuwa kumekuwa na uhusiano mzuri na Tanzania lakini pia kwa hatua ambazo zinachukuliwa na serikali katika kuweka mazingira mazuri ya biashara,’’ alisema Balozi Sjoberg.
Mkurugenzi Mtendaji wa REPOA, Dkt. Donald Mmari alisema taasisi yake itaendelea kufanya tafiti zenye weledi mkubwa ili kuisaidia serikali iweze kufikia malengo ambayo imejiwekea.
‘’Ripoti imeonesha maeneo mbalimbali ambayo serikali imefanya vizuri na pia tumeonesha changamoto ambazo tunaamini zikifanyiwa kazi mazingira ya biashara yatakua na tutawaleta pamoja wadau wa maendeleo (serikali na sekta binafsi,’’ alisema Dkt. Mmari.
Ripoti hiyo inaonesha kuwa nchi za Nordic zimewekeza katika sekta zaidi ya 20 zikiwemo viwanda na mawasiliano na hivyo kuchangia kwa kiasi kikubwa katika utoaji ajira na kukuza uchumi wa Tanzania.
BARAZA la Taifa la Biashara (TNBC) limepokea ripoti iliyoandaliwa na Taasisi ya Utafiti ya REPOA kwa kushirikiana na nchi za Sweden,Denmark, Norway na Finland inayoeleza hali ya uwekezaji na mazingira ya biashara kwa nchi hizo hapa nchini na kuahidi kuyafanyia kazi mapendekezo yaliyomo.
Akizungumza katika hafla ya makabidhiano ya ripoti hiyo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam, Katibu Mtendaji wa wa TNBC, Dkt Godwill Wanga alisema kuwa tafiti zenye weledi zinazoelezea hali ya mazingira ya biashara na uwekezaji zinachagia kwa kiasi kikubwa katika kutatua changamoto zilizopo na kuweka mazingira mazuri zaidi ya kibiashara.
“Leo tumepokea ripoti kutoka REPOA ambayo inaeleza namna serikali ilivyofanikiwa kuweka mazingira rafiki na kuwezesha biashara na uwekezaji pamoja na kutaja maeneo ambayo bado changamoto,’’ alisema Dkt. Wanga na kuongeza kuwa serikali imedharia kuhakikisha kuwa mazingira ya biashara yanaendelea kuimarika na kuvutia wawekezaji zaidi.
Dkt. Wanga alisema kuwa licha ya jitihada kubwa zilizochukuliwa na serikali katika kuweka mazingira rafiki ya ufanyaji biashara Tanzania, zipo baadhi changamoto ambazo serikali kupitia Baraza zinaendelea kuzifanyia kazi.
“Kumekuwepo na jitihada kubwa za serikali katika kuweka mazingira rafiki ya biashara ikiwemo punguzo la tozo mbalimbali pamoja na ushirikiano wa serikali na sekta binafsi.Pamoja na hayo yote mazuri changamoto hazikosekani hivyo kupitia baraza zitaendelea kutatuliwa ,’’ alieleza.
Ameahidi kuwa serikali itafanyia kazi ripoti hiyo kwa kupata majibu ya chagamoto zilizopo hasa kwenye upande wa kodi, uhamiaji hasa upatikanaji wa vibali vya kufanya kazi hapa Tanzania, ubora wa bidhaa pamoja na utaalam.
Kwa Upande wake Balozi wa Sweden nchini Tanzania Balozi Anders Sjoberg alisema, licha ya changamoto zilizopo wataendelea kuita wawekezaji kuja kuwekeza Tanzania kwa kuwa mazingira yanayojengwa sasa ni mazuri lakini sababu nyingine ni mahusiano mazuri kihistoria baina ya nchi hizo.
“Mazingira ya biashara Tanzania ni mazuri licha ya changamoto zilizopo, tunaamini watu wetu wataendelea kuja kuwekeza na kufanya biashara kwa kuwa kumekuwa na uhusiano mzuri na Tanzania lakini pia kwa hatua ambazo zinachukuliwa na serikali katika kuweka mazingira mazuri ya biashara,’’ alisema Balozi Sjoberg.
Mkurugenzi Mtendaji wa REPOA, Dkt. Donald Mmari alisema taasisi yake itaendelea kufanya tafiti zenye weledi mkubwa ili kuisaidia serikali iweze kufikia malengo ambayo imejiwekea.
‘’Ripoti imeonesha maeneo mbalimbali ambayo serikali imefanya vizuri na pia tumeonesha changamoto ambazo tunaamini zikifanyiwa kazi mazingira ya biashara yatakua na tutawaleta pamoja wadau wa maendeleo (serikali na sekta binafsi,’’ alisema Dkt. Mmari.
Ripoti hiyo inaonesha kuwa nchi za Nordic zimewekeza katika sekta zaidi ya 20 zikiwemo viwanda na mawasiliano na hivyo kuchangia kwa kiasi kikubwa katika utoaji ajira na kukuza uchumi wa Tanzania.
Comments
Post a Comment