Makamba aiambia Bodi ya NEMC: komesha rushwa na vyeti feki

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira January Makamba(kushoto) akimkabidhi vitendea kazi Mwenyekiti mpya wa Bodi ya Baraza la Usimamizi na Uhifadhi wa Mazingira(NEMC), Prof. Esnati Chaggu(kulia) katika hafla fupi ya uzinduzi wa bodi hiyo  iliyofanyika jijini Dar es salaam jana.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira January Makamba(kushoto) akimkabidhi vitendea kazi Mmmoja wa wajumbe wa Bodi ya Baraza la Usimamizi na Uhifadhi wa Mazingira(NEMC), Prof. Dos Santos Silayo katika hafla fupi ya uzinduzi wa bodi hiyo iliyofanyika jijini Dar es salaam jana. 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira January Makamba(kushoto) akizungumza jambo na Mwenyekiti mpya wa Bodi ya Baraza la Usimamizi na Uhifadhi wa Mazingira (NEMC), Prof. Esnati Chaggu(kulia) mara baada ya kuzindua bodi hiyo jijini Dar es salaam jana. Wapili kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dkt.Samwel Gwamaka na Wapili kulia ni Mjumbe wa Bodi Prof. Dos Santos Silayo.

 Jackson Kulinga, Dar es Salaam

WAZIRI wa Nchi katika Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Bw January Makamba, jana ameitaka bodi mpya ya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kudhibiti rushwa inayoendekezwa na wafanyakazi na baraza na utoaji wa vyeti feki.

Akizundua bodi hiyo Jijini Dar es Salaam, Waziri Makamba ameitaka bodi isimamie NEMC ili mchakazo wa tathimini ya athari ya mazingira (TAM) ufanyike haraka na uwe wa ubora unaotakiwa. NEMC, ameiambia bodi, inakabiliwa na jukumu kubwa la kupitia maandiko ya miradi na ripoti za TAM ambazo ni nyingi sana kwa sasa.

Waziri amesema: “Nasisitiza sana kuwa, tujitahidi kuepuka migogoro inayosababishwa na utoaji wa vyeti vya mazingira katika maeneo ambayo hatimaye yanasababisha malalamiko.  Pia bodi ihakikishe matatizo ya rushwa miongoni mwa wafanyakazi pamoja na uotaji wa vyeti feki
hayajitokezi tena.”

Waziri huyo amekumbusha kuwa hifadhi ya mazingira siyo tu ni agenda ya kitaifa na kimataifa inayobadilika kwa kasi kubwa bali ni suala la kiufundi. Ameitaka bodi ihakikishe NEMC inakuwa na wataalamu wa kutosha na wenye ujuzi katika fani zinazotakiwa. 
 Ametaja changamoto zinazoendela kwa kasi kuwa mabadiliko ya tabianchi, mmomonyoko wa
utando wa tabaka la ozoni, viumbe vilivyobadilishwa vinasaba (GMOs) na kuenea kwa jangwa.

Pia NEMC iratibu na kufanya taifiti  zinazolenga kutoa suluhisho la matatizo ya mazingira nchini, na kuhakikisha shughuli za maendeleo zinafanyiwa tathimini ya athari ya mazingira na unafanyika utuatiliaji. 
 Ametaka bodi itoe maoni  katika mchakato wa kupata sera mpya ya mazingira inayofikiriwa.
Ametaka bodi ilisaidie baraza kupanua wigo wa mapato kwani, amesema, sasa hivi vyanzo vya makusanyo ni  vichache ikilinganishwa na vile vilivyopo kisheria. NEMC inajiendesha kutokana na mapato yake.

Ametaka NEMC ianzishe kanda ya magharibi ili iwe na kanda saba. Waziri amegusia uhaba wa utaalamu katika fani za gesi, mafuta na madini na kuitaka bodi isimamie baraza kujenga uwezo wa kukabiliana na changamoto hii na zingine.  Sasa hivi NEMC ina wafanyakazi 150.

Amekumbusha kwamba mafanikio ya NEMC   katika utekelezaji wa shughuli za hifadhi ya mazingira unatemea sana uwezo na uelewa wa wadau ambao sasa hivi ni mdogo.  Ameitaka bodi ihakikishe NEMC inaendeleza juhudi ya kujenga uwelewa wa wadau ili washiriki vizuri katika kuhifadhi mazingira.

Mwenyekiti wa Bodi, Profesa Esnati Osinde Chaggu ameahidi kwamba utakuwepo ushirikiano baina ya bodi, NEMC, wizara na wadau.


Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dkt Samuel Gwamaka Mafwenga, ameahidi mabadiliko makubwa ya kiutendaji na kusema baraza litapambana na wanaoendesha shughuli za kibinadamu katika vyanzo vya maji.

“Tutasimamia sheria na kanuni za mazingira bila woga wala upendeleo kwa mtu au taasisi yeyote,”alisema Dkt. Gwamaka na kuahidi kufanya
kazi kwa karibu sana na bodi pamoja na timu ya mejimenti.

Mbali ya Prof. Chaggu, wajumbe wengine waliopo kwenye Bodi hiyo iliyoteuliwa hivi karibuni na Rais Magufuli ni Dkt. Flora Tibarazwa, Prof. Hussein Sosovele, Dkt. Catherine Masao, Bw. Damas Masologo, Dkt. Neduvoto Mollel, Prof. Dos Santos  Silayo, Dkt. Mwakalukwa Ezekiel na
Prof. William Mwegoha.

Mwisho.

Comments

Popular posts from this blog

Tanzania praised for being keen on fertilisers going to farmers

Gold mine in Songwe wins ministerial praise for protecting environment

NEMC warns on emptying effluent in built-up areas, flood waters