NEMC yahimiza uhifadhi wa mti wa msandali
NEMC yahimiza uhifadhi wa mti wa msandali
Na Mwandishi wetu,Manyara
Baraza la Taifa la Uhifadhi wa Usimamizi wa Mazingira(NEMC)
limetoa wito kwa watanzania kujikita katika upandaji wa miti ya misandali kwa
lugha ya kitaalum ‘Osyris
lanceolata’ ikiwa ni sehemu ya kutunza mazingira na pia fursa ya
biashara kutokana na umuhimu wa miti hiyo katika kuzalisha bidhaa mbalimbali.
Akizungumza na waandashi wa habari mara baada ya kutembelea
kiwanda cha kuzalisha mafuta ya
kutengenezea manukato cha Sierra limited kilichopo mkoani Manyara, Mwenyekiti
wa Bodi ya NEMC, Prof.Esnat Chaggu alisema kunaumihimu kubwa wa kupamba miti ya
aina tofauti tofauti kutokana na faida zake kimazingira na kiuchumi pia.
“Hii ni fursa kwa vijana kujikita katika kupanda mashamba ya
miti ya misandali ambayo faida yake kwa baade ni kubwa kutokana na uhitaji
mkubwa wa mti huo katika kuzalisha malighafi ya kutengenezea manukato,” alisema
Prof.Chaggu
Alisema uwekezaji wa aina hii kwa vijana unawaletea faida
kubwa kiuchumi mara baada ya kuivuna na pia mazingira yatakuwa yanaendelea
kulindwa hali ambayo itapelekea ustawi wa nchi kimazingira kuimalika na pia
kiuchumi.
“Ni muhimu kuhamasisha watanzania nchini kupata mti wa
msandali na aina nyinginezo ambayo inafaida kubwa katika matumizi yake, kwani
kwa kufanya hivyo tutakuwa tunaendelea kuongeza idadi ya miti hii kuwa mingi
nchini,” alisema Prof.Chaggu
Aiongezea kuwa tafiti
zinaonyesha kupungua kwa mti huu kutokana na umuhimu wake mkubwa katika
kutengeneza dawa za maradhi mbalimbali kwa binadamu na pia kutengeneza mafuta
yanayotumika kuzalisha manukato hivyo kama wadau wa mazaingira wanalazimika
kuhamasisha upandaji wa miti hii ili kuiendeleza na kuja kusaidia vivazi
vijavyo.
“Nchi yetu ina maeneo mengi ambayo tunaweza kupanda miti ya
aina ya msandali kwa lengo la kuongeza idadi ya miti hiyo nchini na pia kuwa
sehemu ya fursa kwa vijana kujipatia kipato kupitia uwekezaji wa miti,” alisema
Kwa upande wake Meneja wa Kiwanda cha Sierra, Bw.Ashish
Upadhaye alisema mti wa msandali una matumizi mengi hasa katika afya ya
binadamu hivyo ni muhimu kama nchi kuweka kipaumbele katika kulinda miti ya
aina hii na pia kuhamasisha upandi wa miti hii ili iongezeke ambapo italeta
faida kubwa ikitumika kama malighafi ya kuzalisha bidhaa.
“sisi ni wazalishaji wa mafuta ya msandali yanatumika katika
kutengeneza dawa ya maradhi mbalimbali kwa binadamu na manukato, hivyo ni
muhimu kuupa kipaumbele mti huu na miti yenye sifa kama hizi kuendelea kupandwa
nchini kwa faida ya baadae,” alisema Bw.Upadhaye
Naye Mjumbe wa Bodi ya NEMC, Dkt. Neduvoto Mollel alisema faida za mti wa
msandali ni nyingi hivyo wajibu wetu kama Baraza ni kusimamia zaidi katika uhifadhi
wa miti ya aina hii kote nchini na pia kuhamasisha upandaji wa miti hii ili
izidi kuongeza.
“imani yangu
kuwa uhamasishaji ukifanyika miti mingi itapandwa nchini na kupelekea kuwa na
akiba kubwa ya miti ya msandali ambayo inafaida
kubwa na muhimu kwa afya ya binadamu,” alisema Dkt.Mollel
Bodi ikiongozwa Mwenyekiti wake pamoja na
watendaji NEMC wamefanya ziara katika mikoa ya Arusha na Manyara ili kujionea
hali ya uhifadhi wa mazingira ilivyo katika maeneo mbali mbali kwenye mikoa
hiyo na hatua za kuchukua katika kufanya usimamizi ili mazingira yabaki kuwa
salama.
Mwisho.
Comments
Post a Comment