Kirenga: Kipaumbele chetu ni mkulima mdogo kupata soko la uhakika
Afisa Mtendaji Mkuu wa Kituo cha kuendeleza kilimo nyanda za
juu kusini mwa Tanzania(SAGCOT) Bw.Geoffrey Kirenga akizungumza jambo na
waandishi wa habari ofisini kwake jijini Dar es salaam katika mahojiano maalum
juu ya namna walivyojipanga kukuza na kuendeleza mnyororo wa thamani katika
mazao ya kipaumbele katika ukanda wa kusini.
Na Mosses Mahundi,Dar es salaam
Kituo cha Kuendeleza
Kilimo Nyanda za Juu Kusini mwa Tanzania (Sagcot) sasa kinaweka kipaumbele
kwenye kuinua mnyororo wa thamani wa mazao ili wakulima wadogo katika
ushoroba wa kusini mwa Tanzania wapate soko la uhakika la mazao yao.
Kauli hiyo imetoliewa
na Afisa Mtendaji Mkuu wa Sagcot, Bw.Geoffrey Kirenga, katika mahojiano
maalumu juu ya utendaji wa taasisi yao katika kipindi cha miezi tisa
iliyopita.
Amesema tasisi
hiyo kwa sasa msukumo wake ni kutumia kongani zake kuongeza mnyororo wa
thamani katika mazao yanayozalishwa ili wakulima washiriki wenye katika
mapinduzi ya kilimo na kilimo kiwa na tija na wakulima washuhudie wenyewe kilimo kinavyowaletea maendeleo.
mapinduzi ya kilimo na kilimo kiwa na tija na wakulima washuhudie wenyewe kilimo kinavyowaletea maendeleo.
Ameyataja mazao hayo
kuwa ni nyanya, chai, viazi mviringo, maziwa na soya na kusema kuwa baada ya
mazao kuyaongezea thamani yamepata soko la uhakika ndani na nje ya Tanzania.
“Nguvu kubwa
tumeielekeza katika kuongeza thamani mazao yanayozalishwa na wakulima katika
ukanda tuliokabidhiwa na taifa, maana lengo ni kumnufaisha mkulima na
shughuli zake za kilimo na kupata maendele yeye na taifa,” ameeleza
Bw.Kirenga, ambaye anaisimamia taasisi inayoratibu ubia baina serikali ya
Tanzania, wawekezaji wa nje na ndani na wadau wa maendeleo wanaoungamkono
juhudi za Watanzania.
Sagcot sasa hivi
imeweka nguvu zake zote kuleta mapinduzi ya kilimo katika kongani za Ihemi,
Mbarali na Kilombero ambazo zinajumuisha mikoa ya Iringa, Njombe, Mbeya, Songwe
na Morogoro. Kongani za Ludewa, Rufiji na Sumbawanga bado zinafanyiwa
maandalizi.
.Ameeleza kwamba
taasisi yake tayari imeunganisha wakulima wadog katika ushoroba wa kusini
mwa Tanzania na wabia hao wamefikisha huduma mbali mbali kwa wakulima na
kufanya uzalishaji ongezeke maradufu. Hakutoa takwimu.
“Kupitia wabia hawa
tumewafikia wakulima wengi na kuwapatia huduma stahiki ikiwemo pembejeo, elimu juu
ya kilimo bora, teknolojia, viuatilivu, pamoja na kuwaunganisha na masoko ya
uhakika ili kuuza mazao yao,” amesema Bw.Kirenga na kufafanua kwamba mapinduzi
yenye mafanikio huambatana na changamoto.
Kazi hiyo haikuwa
ndogo wala nyepesi, ameeleza mtaalamu huyo wa kilimo, na kusema kuwa Sagcot
ilipoanza jitihada ya kumuinua mkulima katika ushoroba huo, changamoto
kubwa ilikuwa ni kwamba wakulima wengi hawakua na elimu ya kilimo bora na
matumizi sahihi ya pembejeo. Kwa hiyo mavuno yalikuwa kidogo na hafifu na mazao
hayakuwa na soko.
“Kwa hiyo kazi yetu
ilikuwa ni kuwatambua wabia sahihi, wadau mbalimbali wa maendeleo na kuwashawishi
tushirikiane nao kuinua wakulima katika ushoroba wetu; wakakubali. Sasa
tumepiga hatua, tija katika uzalishaji mazao imeongezeka, wakulima wanatuamini
na wao wanajiamini; kwa hiyo tuna msingi imara wa kuchagiza ujenzi wa
viwanda. Viwanda ni soko zuri na salama la mazao ya wakulima na ndiyo maana tunakazana kuyaongezea thamani mazao yao,” amefafanua
viwanda. Viwanda ni soko zuri na salama la mazao ya wakulima na ndiyo maana tunakazana kuyaongezea thamani mazao yao,” amefafanua
Bw.Kirenga ameeleza
kwamba taasisi yao inakazania kuyaongeza thamani ikiwa ni mchango wa
Sagcot kuunga mkono juhudi ya serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais
John Magufuli ya kujenga uchumi wa kati na viwanda ifikapo mwaka
2025. “Sekta ya kilimo ndio kiungo katika kuchagiza azma ya serikali
kufanikiwa.”
Mkuu wa Kongani
na Maendeleo ya Ubia, Bi.Maria Ijumba, ameleza kuwa ongezeko la mazao katika
ushoroba wa kusini kimsingi ni matokeo ya kutumia mbinu ya kongani.
Ameeleza kuwa suala la
kuwaunganisha wakulima wadogo na kuwafikishia huduma ili kilimo kiwe na
tija kwao lilihitaji ubunifu ndiyo sababu tasisi yao ikabinu mbinu ya kongani.
.
“Mfumo wa kongani
umeleta mafanikio makubwa kwa taifa. Umetusiaidia. Imewezekana
mnyororo wa thamani wa mazao ya kipaumbele kufanyiwa kazi kikamilifu na
mazao yamepata masoko ya uhakika ndani na nje ya nchi,” ameeleza.
![]() |
Comments
Post a Comment