DC: Tumia mbolea kunufaika na uchumi wa kati


 Na Abdallah Luambano, Kigoma   

Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Samson Anga amewaomba wakulima wa wilaya na mkoa wa Kigoma watumie mbolea ya bure ambayo imetolewa na Yara kuinua kilimo ili wawe wanufaikaji wa kweli wa uchumi wa kati.

“Nawaomba wakulima wetu wote wachangamkie fursa hii; mbolea ni ya bure. Tukitumia mbolea hii kwa mafanikio  mazao yataongezeka, tutakuwa na hakika ya chakula na tutakuwa sehemu ya uchumi wa kati wa taifa letu,” ameeleza DC Anga.

Mkoa wa Kigoma una wanachi wapatao 2,305,894 (makadirio ya 2015). Ardhi  inayolimwa ni hekta 1,058,637 au asilimia  57.7  ya ardhi yote inayofaa kwa kilimo.  Mkoa unapata mvua nzuri kati ya milimita 600-1,000 kwa mwaka na mazao ya chakula ni mahindi, muhogo, mtama, viazi, ndizi na maharage.  Mkoa wa Kigoma ni asimilima 4.8 ya Tanzania Bara na shughuli kuu za uchumi ni kilimo, uvuvi na uchakataji wa samaki viwandani.

DC Anga amewaomba wakulima wajenge tabia ya kutumia mbolea kwa ufanisi na hasa kwa vile Yara imetoa mbolea ya bure kuinua kilimo cha mahindi n mpunga.  

Kampuni ya   Yara International, imeamua kugawa mbolea bure  kiasi cha tani  elfu 12 na nusu kwa wakulima wadogo wa Tanzania ili kuimarisha usalama wa chakula katika ngazi ya kaya na taifa kwa jumla.  Mbolea iniliyotolewa inakadiriwa kuwa na thamani ya bilioni 16.5/=.  Kampuni hiyo imetoa mbolea kwa nchi mbali mbali za Afrika, katika mpango wake unaoitwa Action Africa.

Wilaya Kigoma, inajumuisha sehemu za vijijini na mjini.  Kigoma Vijijini ina watu 489,271 na Manispa ya Kigoma ina watu 144,256.

Serikali inapigana kuinua pato la mwananchi wa kawaida wa Kigoma kutoka 1,152,553/=  (makadirio ya 2016) kwa mwaka kwa kutumia kilimo ili wazalishe mazao yenye soko la ndani na nchi za jirani za Jamhuri ya Watu wa Kongo, Zambia, Burundi na Rwanda.
Kilimo ni uti wa mgongo wa uchumi wa Mkoa wa Kigoma na asilimia 80 za shughuli za  kiuchumi zinatokana shughuli za kilimo.

Meneja Biashara wa YARA Kanda ya Ziwa, Bw. Phillipo Mwakipesile amewahimiza wakulima kujisajili  kwa kupiga *149*46*16#.

"Huu mpango wa kugawa mbolea bure ni dhamira ya kweli ya YARA kuwainua wakulima wadogo hapa nchini," alisema na kuongeza kuwa hauna uhusiano na masuala ya siasa.



Comments

Popular posts from this blog

Set aside land for investment, Kairuki tells RCs,district councils

Mkuu wa Mkoa Pwani asifu juhudi za mmiliki wa Makampuni ya Global Packaging na Wande Printing

17 projects to house 80,000 tonnes of crops being built