Waziri Sima: NEMC haitakuwa kikwazo kwa wawekezaji


NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Bw. Mussa Sima akizungumza na waandishi wa habari mkoani Mtwara hivi karibuni jinsi Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) ambalo lipo chini ya Ofisi yake kwa namna linavyopambana kuweka mazingira rafiki ili kuendelea kuwavutia wawekezaji hapa nchini.


NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Bw. Mussa Sima akizungumza na waandishi wa habari mkoani Mtwara hivi karibuni jinsi Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) ambalo lipo chini ya Ofisi yake kwa namna linavyopambana kuweka mazingira rafiki ili kuendelea kuwavutia wawekezaji hapa nchini.

Waziri Sima: NEMC haitakuwa kikwazo kwa wawekezaji
Na Mwandishi Wetu, Lindi

NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Bw. Mussa Sima amelipongeza Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) ambalo lipo chini ya Ofisi yake kwa namna linavyopambana kuweka mazingira rafiki ili kuendelea kuwavutia wawekezaji hapa nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari katika ziara yake mkoani Mtwara, Bw. Sima amesema kuwa licha ya changamoto zilizopo, ofisi yake imeendelea kufanyia kazi mabadiliko mbalimbali ya kanuni na sheria ili kwenda sambasamba na azma ya serikali ya ujenzi wa uchumi wa kati na viwanda pasipo kuathiri mazingira.

“Tunapozungumzia mazingira tunazungumzia juu ya uhai wetu, hivyo kama Wizara yenye jukumu la kusimamia mazingira tunalazimika kusimamia ustawi wa jamii bila kuathiri uwekezaji,” alisema Bw. Sima
Bw. Sima amesema kuwa tayari ofisi yake imechukua hatua kadhaa ikiwemo kurekebisha baadhi ya tozo hali ambayo imepunguza malalamiko mengikutoka kwa  wawekezaji.

‘’Huko nyuma tulikuwa tukitoza asilimia moja ya jumla ya mradi au biashara lakini sasa tumeganya miradi ambapo kila mradi  utakuwa na tozo yake. Mfano huko nyuma wamiliki wa visima vya mafuta walikuwa wanatozwa mpaka milioni 10 lakini kwa marekebisho ya sasa watakuwa na
tozo ya milioni 4,’’ alisema Bw. Sima.

Sima aliongeza  changamoto nyingine kuwa ni  uchelewashaji wa Tathmini ya Athari kwa Mazingira (EIA) ambapo ilikuwa inachukuwa siku 149 lakini kwa marekebesho ya kanuni yaliyofanywa mwezi Septemba, 2018 yalipunguza siku hizo na kuwa 95 tu.

“EIA ilikuwa inachukua muda mrefu sana na badaa ya kutafakari kwa kina, tuliamua kufanya mabadiliko ya kanuni ambapo tumetoka siku 149 na sasa zimekuwa siku 95 hali ambayo inaonyesha ni kwa namna gani tumelenga kurahisisha uwekezaji,’’ alifafanua Bw. Sima na kuongeza

“Tatizo la ucheleweshwaji wa EIA sio tatizo la NEMC bali ni la Wataalamu Elekezi ambao wamekuwa na namna yao katika utekelezaji wa miradi, hata hivyo tumeshakutana na tumeweka utaratibu wa tozo ambao unawiana na ule wa serikali,”


Aidha alitumia nafasi hiyo kueleza mchango wa Wakaguzi wa Mazingira ambao wapo kila mkoa kwa namna wanavyofanya kazi nzuri lakini hawawezi kufanya nje ya utaratibu za mikoa.

“Natoa rai kwa wakaguzi wa mazingira kote nchini kutengeneza mpango kazi na kuukabidhi   ofisi ya mkoa ili watambulike wanafanya kazi gani kwani hawa ni wadau muhimu sana katika mazingira na tuliwatumia wakati wa utekelezaji wa katazo la ututumiaji wa mifuko ya plastiki,” alisema

Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) kupitia Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) wameendelea kuchukua hatua madhubuti katika kuhakikisha utekelezaji wa azma ya serikali ya uchumi wa viwanda inatekelezeka pasipo kuathiri mazingira.




Comments

Popular posts from this blog

Set aside land for investment, Kairuki tells RCs,district councils

Mkuu wa Mkoa Pwani asifu juhudi za mmiliki wa Makampuni ya Global Packaging na Wande Printing

17 projects to house 80,000 tonnes of crops being built