Rais,Dkt.John Pombe Magufuli amepongeza Kampuni ya Unilever Tea Tanzania kwa kujenga kiwanda cha kisasa cha kuchakata majani ya chai Mkoani Njombe

Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli (kushoto) akimsikiliza kwa makini Mkurugenzi Mkuu wa Unilever Tea Tanzania Bw.Ashton  Eastman wakati wa Uzinduzi wa Kiwanda cha kuchakati chai cha Kabambe ambaco ni moja ya viwanda vinavyomilikiwa na Unilever Tanzania.
Mkurugenzi Mtendaji wa Unilever Tanzania,Bwana David Minja akisoma hotuba yake Mbele ya Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli wakati wa Uzinduzi wa Kiwanda cha kuchakati chai cha Kabambe ambaco ni moja ya viwanda vinavyomilikiwa na Unilever Tanzania.
Na Mwandishi wetu,Njombe.
Rais,Dkt.John Pombe Magufuli amepongeza Kampuni ya Unilever Tea Tanzania kwa kujenga kiwanda cha kisasa cha kuchakata majani ya chai Mkoani Njombe, nakuwataka watendaji Serikali kupunguza urasimu na vikwazo kwa wawekezaji wanaotaka kuwekeza nchini jambo linalopelekea kuchelewa maendeleo.
Ameyasema hayo mkoani hapa alipokuwa katika uzinduzi wa kiwanda cha chai cha Kabambe  ikiwa ni sehemu ya mwendelezo wa ziara yake katika mikoa ya Kusini na Nyanda za Juu kusini mwa Tanzania na kuwataka  watendaji wa Serikali kutowabugudhi wawekezaji wenye nia ya kuwekeza nchini.
“Tumekuwa tukirudi nyuma kimaendeleo kutokana na urasimu wa baadji ya watendaji Serikali hali inayopelekea kuchelewa kufikia malengo tuliyojiwekea kama Serikali, hivyo niwatake watendaji wote kutekeleza majukumu yao pasipo kuleta urasimu,” Alisema Rais Magufuli
Alisema mwekezaji atakayekwamishwa na mtendaji yoyote wa Serikalini atoe taarifa katika ofisi yake ili hatua za kinidhamu zichukuliwe dhidi ya huyo mtumishi ambaye anakuwa kikwazo cha uwekezaji nchini.
“Lazima watu wawajibishwe kwa vitendo vya urasimu vinavyopelekea Nchi yetu kuonekana inavikwazo vingi katika uwekezaji, ijapokuwa  watu wachache ndio wanasababisha mazingira hayo kwa sababu ya rushwa,”alisema Rais Magufuli
Aliongezea kuwa Serikali inapaswa kuandaa mpango kazi utakaotoa mwongozo wa namna bora ya kulinda mazingira ya uwekezaji nchini na mikakati ya kuvilinda viwanda vitakavyo jengwa kama cha Kabambe cha kuchakata chai.
“Zaidi ya Bilioni 49 zimewekezwa katika kiwanda hiki hivyo ni lazima kuwe na mazingira bora ya kukilinda kiwanda hichi kwa hali yoyote ili kiendelee kuotoa ajira kwa watanzania na kupeleke azma ya Serikali ya kujenga viwanda kutekeleza kwa vitendo,” alisema Rais Magufuli
Aidha, Alipongeza Ubalozi wa Uingereza nchini, The Wood Foundation, Kaibu Mkuu Kiongozi Mstaafu Balozi Philemon Luhanjo, Spika wa Bunge Mstaafu Mama Anna Makinda, Kituo cha Kuendelea Kilimo Nyanda za juu kusini mwa Tanzania(SAGCOT) kwa kuwezesha kuwepo kwa kiwanda hicho mkoani Njombe.
“Niwatake wakulima wa chai mkoani Njombe kulima zao hili kwa wingi kutokana na uwepo wa kiwanda cha kisasa cha kuchakata chai zaidi ya tani elfu 150 ambapo asilimia 70 ya majani mabichi yanategemewa kutoka kwa wakulima hali inayoibua fursa ya soko la majani mabichi, ,” alisema Rais Magufuli
Alisema kiwanda cha Kabambe kitapelekea kipato kwa mkulima mdogo kuongezeka na kuchochea ukuaji wa uchumi wa mkoa na taifa kwa ujumla kupitia kodi zitakazolipwa na kiwanda , hali itakayopelekea nchi kupiga hatua kiuchumi.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Unilever Tanzania,Bwana David Minja alisema kampuni imetoa ajira zaidi ya watanzania elfu 7 na kunufaisha watuzaidi ya elfu 40 kupitia kampuni za Unilever Tanzania kikiwepo kiwanda cha kuchakata chai cha Kabambe.
“Tumejipanga katika kutoa mafunzo na elimu ya kilimo bora cha chai ili wakulima waweze kulima chai yenye ubora utakao kubalika na kupelekea soko la chai kuwa nzuri na kuwanufaisha wakulima kwa kupata vipato vya juu,” alisema Bw.Minja
Alisema changamoto kubwa ni miundombinu ya barabara ya kutoa chai mashambani na kufikisha kiwanda kwa wakati hali inayopelekea chai nyinig kuharibika kabla ya kufika kiwanda kwa ajili ya kuchakatwa hivyo kumpelekea mkulima hasara.
naye Balozi wa Uingeraza nchini Tanzania Bi.Sarah Cooke alisema kufanikiwa kwa uwepo wa kiwanda cha kuchakata chai kutachochea wawekezaji wengi zaidi kutoka Uingereza kuja kuwekeza Tanzania nah ii ni kutoakana na uongozi mzuri wa Rais Dkt.John Magufuli katika kusimami sera ya Viwanda.
“Maendeleo yanaletwa na viwanda hivyo kuwepo kwa viongozi waadilif, mazingira bora na mikakati ya uwekezaji  kutachochea wawekezaji wengi kuja kuwekeza Tanzania, “ alisema Balozi Cooke
Mwisho.

Comments

Popular posts from this blog

Mkuu wa Mkoa Pwani asifu juhudi za mmiliki wa Makampuni ya Global Packaging na Wande Printing

17 projects to house 80,000 tonnes of crops being built

Tanesco: Azma ya uchumi wa kati na wa viwanda ifikapo 2025 inatekelezeka