Tanesco: Azma ya uchumi wa kati na wa viwanda ifikapo 2025 inatekelezeka
Na
jenny Chillery, Dar es Salaam
Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) limesema kuwa usambazaji wa umeme vijijini unabadilisha maisha ya wananchi na umekuwa ni chocheo kikubwa katika kutimiza azma ya serikali ya Rais John PombeMagufuli ya kuifanya Tanzania kuwa nchi ya uchimi wa kati na wa viwanda ifikapo 2025.
Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) limesema kuwa usambazaji wa umeme vijijini unabadilisha maisha ya wananchi na umekuwa ni chocheo kikubwa katika kutimiza azma ya serikali ya Rais John PombeMagufuli ya kuifanya Tanzania kuwa nchi ya uchimi wa kati na wa viwanda ifikapo 2025.
Akizungumza katika mahojiano na katika kipindi kilichorushwa na Kituo kimoja cha Television Jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Dkt. Tito Mwinuka, amesema jana kuwa Tanesco imekuwa ikishirikiana kwa karibu sana na Wakala wa Usambazaji Umeme Vijijini (REA) katika kupeleka umeme vijijini. Ameshukuru REA kwa ushirikiano huo na kueleza kuwa ushirikiano huo umeongeza sana ujenzi wa viwanda vya kati, na kwamba ujenzi wa viwanda umesaidia sana katika kubadili
maisha
ya wananchi kiuchumi.
Kwa kuwa umeme umefika vijijini, ameeleza mtaalamu huyo, azima ya kufikia uchumi wa kati na wa viwanda ifikapo 2025 inatekelezeka. Amesema katika kipindi cha miaka minne iliyopita Tanesco imeunganisha zaidi ya vijiji 300 na umeme wa gridi.
“Tunawashukuru sana wenzetu wa REA kwa namna tunavyoshirikiana katika kusambaza umeme katika vijiji vya Tanzania. Kuwepo kwa umeme kukewafanya wawekezaji wajenge viwanda vya kati na jambo hilo limeinua uchumi wa wananchi,” amesema kiongozi huyo.
Dk Mwinuka ametaja moja ya mafanikio makubwa ya Tanesco katika miaka minne ya iliyopita kuwa ni kuiunganisha mikoa ya Njombe na Ruvumakwenye gridi ya taifa.
“Tanesco imejitihidi kuunganisha maeneo mengi na gridi ya taifa. Kuunganisha mikoa ya Njombe na Ruvuma na gridi ya taifa, kumeiwezesha serikali kuokoa zaidi ya shilingi bilioni 25, fedha ambayo imekuwa ikitumika kununulia mafuta mazito ya kuendesha majenereta,” ameeleza.
Dk. Mwinuka ameishukuru serikali kwa kuiunga mkono Tanesco katika kutekeleza mradi wa umeme wa Kinyerezi II, na kueleza kuwa mradi huo unachangia megawati 248 kwenye gridi ya taifa.
“Tanesco hatutakubali kuwa nyuma katika kuleta mageuzi ya kiuchumi hapa nchini. Tunataka kuona umeme unakuwa kiunganishi muhimu katika ujenzi wa viwanda na uchumi wa kati ifikapo 2025. Tutajitahidi kuona wananchi wanapata umeme kwa gharama nafuu, hasa wanyonge, ili wafaidi matunda ya nchi yao.”
Mwisho.
Comments
Post a Comment