Mkuu wa Mkoa Pwani asifu juhudi za mmiliki wa Makampuni ya Global Packaging na Wande Printing

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarist Ndikilo(kushoto) akizungumza jambo na Mwakilishi wa Makampuni ya Global  Packaging Ltd na Wande Printing Ltd Bw. Benno Mwitumba(wapili kulia) na wadau wengine katika eneo la ujenzi wa ukumbi na ofisi  za chama  cha mapinduzi (CCM) mkoa wa Pwani  unajengwa  kwenye ofisi za  CCM Mkoa mara baada ya kukabidhiwa mifuko ya 200 ya saruji.

Mkuu wa Mkoa wa Pwani , Mhandisi Evarist Ndikilo  (kulia) akizungumza  mara baada ya kumalizika kwa hafla fupi ya makabidhiano ya mifuko 200 ya saruji  iliyofanyika  kwenye makao makuu ya Chama cha Mpinduzi Mkoani Pwani  lengo ikiwa ni  kusaidia ujenzi wa ukumbi na ofisi ya Chama hicho. Wapili kulia ni  mwakilishi wa Makampuni ya Global  Packaging Ltd na Wande Printing Ltd Bw. Benno Mwitumba, kushoto ni  mshauri wa Uchumi  kutoka Global  Packaging Ltd Bw. Adoh Mapunda na wapili kushoto ni  Katibu Mkuu wa CCM Mkoa wa Pwani, Bw. Ally Makoa.


Mkuu wa Mkoa wa Pwani , Mhandisi Evarist Ndikilo  (kulia) akizungumza  mara baada ya kumalizika kwa hafla fupi ya makabidhiano ya mifuko 200 ya saruji  iliyofanyika  kwenye makao makuu ya Chama cha Mpinduzi Mkoani Pwani  lengo ikiwa ni  kusaidia ujenzi wa ukumbi na ofisi ya Chama hicho. Wapili kulia ni  mwakilishi wa Makampuni ya Global  Packaging Ltd na Wande Printing Ltd Bw. Benno Mwitumba, kushoto ni  mshauri wa Uchumi  kutoka Global  Packaging Ltd Bw. Adoh Mapunda na wapili kushoto ni  Katibu Mkuu wa CCM Mkoa wa Pwani, Bw. Ally Makoa.

Mkuu wa Mkoa Pwani asifu juhudi za mmiliki wa Makampuni ya Global Packaging na Wande Printing
Na Abdallah Luambano, Kibaha
Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarist Ndikilo amemmwagia sifa mmiliki wa Kampuni ya Global Packaging na Wande Printing and Packaging  Ltd, Bw. Joseph Wasonga katika jitihada zake za kuchangia shughuli za maendeleo  mkoani humo.
Akizungumza na waandishi wa habari katika hafla fupi ya makabidhiano ya mifuko 200 ya saruji kusaidia ujenzi wa ukumbi na ofisi ya Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Pwani mjini Kibaha, Mkuu wa Mkoa, Mhandisi Ndikilo amesema kuwa Mwenyekiti wa Makampuni hayo amekuwa mfano wa kuigwa katika kuchagiza maendeleo katika mkoa wake.
"Kwa kipekee kabisa napenda kumshukuru Mwenyekiti wa Makampuni ya Global na Wande Printing kwa namna anavyojitoa katika kutimiza malengo ya chama na serikali mkoani hapa jambo linapaswa kuigwa na kila mwekezaji na wadau wote wa maendeleo,’’ alisema Mhandisi Ndikilo.
Akiongea kuhusu mchango wa mifuko 200 ya saruji ambayo ilikabidhiwa kwa Ofisi ya CCM Mkoa wa Pwani, alisema kuwa ujenzi wa ukumbi na ofisi za mkoa utaongeza fursa katika Mkoa wa Pwani.
“Mchango huu kwa CCM Mkoa ukitumika vizuri na hatimaye kukamilika kwa ujenzi wa ukumbi na ofisi utachangia sana kuongeza fursa za ajira, kuongezeka kwa mapato na kuendelea kuimarika kwa CCM ndani ya Mkoa wa Pwani,’’ alisema Mkuu wa Mkoa.
Aidha, Bw. Ndikilo alitoa mwito kwa wadau wengine wa chama na serikali kuendelea kuchangia ujenzi wa ukumbi huo kwani bado upo katika hatua za awali.
‘’Nitoe wito kwa wadau wa chama kuendelea kuchangia ujenzi wa ofisi hizi kama ambavyo Katibu Mkuu wa CCM Taifa Bwana Bashiru Ally amekuwa akisisitiza kwamba watu wa chama waone fahari kuchangia maendeleo ya chama chetu, Bwana Wasonga kaanza na wengine tufuate,’’ alisisitiza Mhandisi Ndikilo.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Global Packaging ambaye alikabidhi mifuko hiyo kwa niaba ya mwenyekiti wa makampuni hayo, Bw. Benno Mwitumba alisifu Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Pwani chini ya Mhandisi Ndikilo kwa namna ambavyo imekuwa ikitoa ushirikiano kwa wawekezaji na wadau wa maendeleo mkoani humo.
‘‘Tunaishukuru ofisi ya mkoa kwa kutuunga mkono na kwa kuweka mazingira rafiki kwa wawekezaji hali ambayo imeturahisishia sana katika kuendesha shughuli za uwekezaji katika viwanda na maeneo mengine ya kijamii,’’ alisema Bw. Mwitumba.
Bw. Mwitumba alisema kuwa watajitahidi kuongeza ushawishi wao kwa kampuni na mashirika mbalimbali ya maendeleo ili kufanikisha ujenzi wa ukumbi kwa wakati.
“Taarifa tulizonazo ni kuwa ukumbi huu unatakiwa kukamilika mwezi wa sita mwakani, kama wadau wa maendeleo kwa kuungana na CCM mkoa tutakuwa mstari wa mbele katika kuwatafuta wadau ili waweze kuchangia na kukamilisha ujenzi huu ndani ya muda uliopangwa,’’ alisema.
Katika hatua nyingine Bw. Mwitumba alimkabidhi mkuu wa mkoa hundi yenye thamani ya shilingi milioni moja kama ada ya ushiriki katika maonesho ya viwanda na kuahidi kutoa mchango wa kuwezesha maonesho hayo yatakayoanza mapema mwezi wa kumi.
Naye Katibu Mkuu wa CCM Mkoa wa Pwani, Bw. Ally Makoa alimshukuru mmiliki wa makampuni hayo kwa namna anavyojitoa katika kuijenga Kibaha katika nyanja mbalimbali na kuwahakikishia kuwa mchango wao utafanya kazi iliyokusudiwa.
Mwisho.




Comments

Popular posts from this blog

17 projects to house 80,000 tonnes of crops being built

Tanesco: Azma ya uchumi wa kati na wa viwanda ifikapo 2025 inatekelezeka