YARA yajizatiti kuchangia uimarishaji wa sekta ya kilimo


Na Abdallah Luambano, Dar es Salaam

Kampuni ya YARA Tanzania imeahidi kushirikiana na serikali kwa karibu sana ili kuhakikisha mpango wa ugawaji mbolea bure kwa wakulima nchini unakuwa wa manufaa kwa wakulima na taifa kwa jumla. 
 
Akizungumza na waandishi wa habari juzi, siku chache  baada ya uzinduzi wa ugawaji wa mbolea uliofanyika Jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo, Bw.Winstone Odhiambo,  alisema mpango huo umelenga kuhakikisha nchi za Afrika ikiwemo Tanzania zinajitosheleza katika kuzalisha chakula.  Kwa upande wa Tanzania mpango huo ni jitihada ya kampuni yao kuchangia jihada ya serikali katika kuimarisha sekta ya kilimo.

Lengo la kampuni ni kuhakikisha  uzalishaji wa mazao hususani mahindi na mpunga unaongezeka katika nchi za Afrika kupitia mradi maalum wa kampuni ujulikanao kama Action Africa,alisema Odhiambo

Alisema mradi wa ugawaji mbolea bure ni moja ya miradi mikubwa ambayo imetekelezwa tangu kampuni kuanzishwa nchini Tanzania miaka 15 iliyopita.

Naishukuru Serikali ya Tanzania, kupitia Wizara ya Kilimo, kwa ushirikiano mkubwa tulioupata ambao umetusaidia kuhakikisha azma ya kampuni yetu inatekelezeka kwa vitendo na pia kwa kufanya tafiti za ubora wa mbolea kupitia mamlaka za uthibiti zilizopo nchini , alisema Odhiambo

Aliongezea kuwa ubora wa mbolea inayotolewa kwa wakulima umezingatia mazingira ya ardhi ya Tanzania na kuongeza kwamba mbolea hiyo  itatibu udongo na kurutubisha aradhi na kwa hiyo mazao yatastawi vizuri na kuongezeka.

Mbolea inayokwenda kwa wakulima ni NPK ambayo ni mahsusi kwa mazao ya mpunga na mahindi, hivyo tani 12,500 zitagagiwa kulingana na vigezo na masharti yaliyowekwa, alisema 

Aidha, Bw.Odhiambo alieleza utaratibu wa kujisajili ili kufanikiwa kupata mbolea hizo ni kupitia namba *149*46*16# kwa mitandao yote ya simu, hivyo wakulima waendelee kujisajili ili waweze kunufaika na mpango huu.

Pamoja na kugawa mbolea kampuni itaendelea kutoa ushauri kwa wakulima juu ya matumizi bora ya pembejeo na mbinu za kisasa za kidigitali za kuongeza uzalishaji ili kuhakikisha nchi inazalisha chakula cha kutosha, alisema Odhiambo 

Alieleza kuwa mpango huo mbali ya kuongeza chakula,  ni sehemu pia ya kuunga mkono juhudi za Serikali ya awamu ya tano nchi ya Rais Dkt.John Magufuli katika kuendeleza kilimo ili kiweze kusaidia katika maono ya nchi ya kufikia uchumi wa viwanda ifikapo 2025.

 

Comments

Popular posts from this blog

Set aside land for investment, Kairuki tells RCs,district councils

Mkuu wa Mkoa Pwani asifu juhudi za mmiliki wa Makampuni ya Global Packaging na Wande Printing

17 projects to house 80,000 tonnes of crops being built