Wajasiriamali wapongeza Mradi wa Viwanda Mbeya

Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Sekta Binafsi Nchini(TPSF) Bi.Angelina Ngalula(kushoto) akipewa maelezo na Mkurugenzi wa Kampuni ya Rohi(Wazalishaji wa bidhaa za ndizi) ,Bi.Rose Muriahela(kulia)  alipotembelea mabanda ya wajasiriamali mara baada ya kumaliza hafla ya makabidhiano ya eneo la hekari 5 lilitolewa na Serikali ya Mkoa wa Mbeya kwa ajii ya kujenga Viwanda vya kusindika chakula.
Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Sekta Binafsi Nchini(TPSF) Bi.Angelina Ngalula(kulia) akipewa maelezo na Bw.Justin Fungo(kushoto) Mjasiriamali wa Glosama Bakers wazalishaji wa mikate alipotembelea mabanda ya wajasiriamali mara baada ya kumaliza hafla ya makabidhiano ya eneo la hekari 5 lilitolewa na Serikali ya Mkoa wa Mbeya kwa ajii ya kujenga Viwanda vya kusindika chakula.

 


Na Moses Mahundi, Mbeya

Wajasiriamali wasindikaji wa mazao ya chakula mkoani Mbeya wakihojiwa Jijini hapa wamepongeza hatua ya ujengaji viwanda vidogo Jijini hapa  katika mradi unaoratibiwa na Taasisi ya Sekta Binafsi  (TPSF).Mradi huo unasimamiwa  Chama cha Wasindikaji Chakula na Mazao(TAFOPA) na kufadhiliwa vikubwa na shika la Uswisi la HELVES.
 HELVETAS imekuwa na ikifadhili Mradi wa Kilimo Bora cha Mboga na Matunda kwa Wanawake na Vijana(KIBOWAVI) na kwa ushirikiano na TPSF viwanda vidogo  na mitambo ya baridi vinajengwa ili kurahisisha usafirishaji wa mazao yanayokubalika masoko ya nchi za nje.
Bw Renatus Lembileki amesema wakulima wanaongeza uzalishaji wa mazao kwa sababu wanasababu ya kufanya hivyo. “Tuna matumaini makubwa sasa na tunaongeza uzalishaji wa mazao.  Tatizo kubwa lilikuwa ni ardhi ya kujengwa viwanda, siyo fedha, au mazao au wakulima… bali ardhi,” ameeleza mtaalamu wa kilimo mstaafu anayelima kabichi na maparachichi.
“Ni rahisi kupata fedha au kwingineko kwa muda mfupi ili kuanzisha viwanda, lakini bila ardhi utaviweka wapi? Hufiki kokote na hivi ndivyo imekuwa kwa muda mrefu,”ameeleza mtaalamu huyo na kufafanua kwamba balaa la ugonjwa wa Corona limeibua masoka mengi yenye kuhitaji bidhaa za kilimo kati nchi za mashariki, kati, kusini mwa Afrika, Ulaya na Marekani. “Jamani watu huko wanahitaji mazao, siyo maneno.”
Bw.Justin Fungo wa Glosama Bakers amesema wajasiriamali wengi watapata sehemu za kuzalisha bidhaa zao na kupata masoko ya uhakika.
“Mradi huu utatuinua wengi kwani mtaji wa kununua mashine za kuchakata bidhaa umekuwa ni tatizo kubwa. Pia mradi utakuwa chachu ya kuongezeka kwa uzalishaji wa bidhaa na kupunguza upotevu wa mazao kwa kukosa soko,” ajmesema Bw.Fungo. Ameipongeza  serikali kwa kutoa ardhi ya kujenga viwanda.
Bi Syana Asalile wa Nuru Asili Farms amesifu mradi na kusema utapunguza uharibifu wa mazao yao ya ufugaji na kilimo cha matunda kwani yatakuwa  yanasindikwa jijini na kutafutiwa masoko ya ndani na nje.
“Kwa muda mrefu nimekuwa nachakata maziwa na natengeza juisi za matunda.  Lakini bidhaa zetu zimekuwa zikiharibika. Mradi huu utakuwa mkombozi kwangu,” amesema Bi.Asalile
Bw Francko Jackson wa Jamii Kyela Products  ameupongeza ufadhili wa  HELVETAS na kusema utawafanya wajasiriamali wengi zaidi kujiajiri na kuongeza kwa ubunifu katika kutengeneza bidhaa.
“Tatizo la uharibifu wa bidhaa lilionekana kama vile halina utatuzi. Kukamilika kwa mradi huu kutatufanya turasimishe bidhaa zetu kwenye mamlaka husika na kufanya bidhaa zetu zikubalike katika masoko ya ndani na nje,” ameeleza.
 Mwenyekiti wa TPSF, Bi.Angelina Ngalula alipotakiwa kutoa maoni yake, amesema  TPSF inafuatilia kwa karibu mradi huo na kuongeza kwamba jitihada ya TPSF ni kutumia katika mikoa mingine uzoefu inaoupata Mkoani Mbeya.
“Tunaendelea kuhamasisha Mikoa mingine nchini kuandaa maeneo kwa ajaili ya ujenzi wa viwanda hivi ili pale miradi itakapokuja iwe rahisi  kutekelezwa.”
Mwisho//

Comments

Popular posts from this blog

Kirenga: Kipaumbele chetu ni mkulima mdogo kupata soko la uhakika

Gold mine in Songwe wins ministerial praise for protecting environment

NEMC warns on emptying effluent in built-up areas, flood waters