Agricom Tanzania yashinda tuzo zana bora za kilimo

Waziri wa Kilimo Bw.Japhet Hasunga(Wapili kushoto) akimkabidhi tuzo mshindi wa kwanza katika eneo la zana za kilimo kwa niaba ya Waziri Mkuu Bw.Kassim Majaliwa,  Kaimu Meneja Mkuu wa Kampuni ya Agricom Tanzania, Bw.Remmy Nindi katika kilele cha sikukuu ya wakulima(nanenane) yaliyifanyika kitaifa mkoani Simiyu hivi karibuni.




Kaimu Meneja Mkuu wa Kampuni ya Agricom Tanzania, Bw.Remmy Nindi akifurahia na wafanyakazi wake katika viwanja vya nanenane nyakabindi Mkoani Simiyu mara baada ya kukabidhiwa tuzo ya  mshindi wa kwanza katika eneo la zana za kilimo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho sikukuu ya wakulima.



Na Mosses Mahundi, Bariadi

KAMPUNI ya Agricom Tanzania ambayo inajihusisha na uuzaji pamoja na ushambazaji wa zana za kilimo hapa nchini imeshinda tuzo ya mshindi wa kwanza katika eneo hilo kwenye sherehe za a Nane Nane zilizofanyika kitaifa mkoani Simiyu mwaka huu.

Akizungumzia tuzo hiyo iliyokabidhiwa na Waziri wa Kilimo,Bwana Japhet Hasunga kwa niaba ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Kaimu Meneja Mkuu wa Agricom, Bw.Remmy Nindi amesema tuzo hiyo imeongeza hamasa kubwa kwa kampuni yake  kuendelea kutoa huduma na  kushiriki kikamilifu kwenye maonyesho kama hayo  kipindi kijacho.

“Tunaishukuru serikali na waandaaji wa tuzo hizi kwani ni chachu kwetu ya kuongeza ubunifu katika utoaji wa huduma na kuwafikia wadau wengi zaidi katika sekta ya kilimo,” alisema Bw.Nindi.

Alisema  zana mbalimbali za kilimo zilizopelekwa kwenye maonesho mwaka huu ni zenye ubora wa hali ya juu na kukidhi marajio ya wakulima katika ngazi zote ndiyo siri kubwa ya kushinda tuzo.

“Kampuni yetu imekuja kuziba pengo la uhaba wa zana za kilimo nchini, kwani tumeweza kufungua ofisi katika baadhi ya mikoa na lengo letu ni kuhudumia kanda zote sambamba nakuwafikishia  huduma wakulima kwa urahisi zaidi,” alisema Bw.Nindi.

Alisema Agricom Tanzania ina ofisi maeneo la Melela mkoani Morogoro kwa ajili ya kuhudumia kanda ya mashariki, Kibaigwa mkoani Dodoma kwaajili ya  mikoa ya kanda kati, Kahama mkoani Shinyanga kwa mikoa yote ya kanda ya ziwa na Igurusi mkoani Mbeya kwa mikoa ya Kanda ya Nyanda za Juu Kusini.

Aidha, Bw.Nindi alisema maonyesho ya mwaka huu yamekuwa na mwitikio kubwa tangu siku ya kwanza ya ufunguzi kwani wananchi wengi wamekuwa wakijitokeza kutembelea banda la Agricom na kujionea zana  mbalimbali za kilimo  zinauzwa na kampuni yake.

“Tumeweza kuuza treka, pawatila na majembe.  Kulingana na mwitikio wa wakulima wengi tunaimani mashine nyingi zitanunuliwa,” alisema Bw.Nindi na kuongezea kuwa Agricom inatoa pia huduma ya kusambaza zana hizo kote nchini bila kujali mkulima anapatikana mkoa gani.

Katika maonyesho hayo, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alipongeza juhudi za Kampuni hiyo katika kuhakikisha zana za kilimo zinapatikana kwa urahisi na wakati hasa katika msimu wa kilimo na kuwezesha  mkulima kufanya kilimo cha kisasa.

“Umefika wakati sasa mkulima kuachana na jembe la mkono na kuanza kutumia zana bora za kisasa yakiwemo matrekta na mashine mbalimbali za kuchakata mazao hali itakayosaidia kuongeza tija katika uzalishaji na kuinua kipato cha mkulima ,” alisema Waziri Mkuu Majaliwa.

Aliwataka wakulima nchini kutumia fursa ya mikopo kutoka katika mabenki washirika ikiwemo Benki ya maendeleo ya kilimo Tanzania (TADB), CRDB, NMB,NBC pamoja na taasisi nyingine za kifedha ili kuongeza uzalishaji.


Comments

Popular posts from this blog

NEMC warns on emptying effluent in built-up areas, flood waters

Set aside land for investment, Kairuki tells RCs,district councils

Mkuu wa Mkoa Pwani asifu juhudi za mmiliki wa Makampuni ya Global Packaging na Wande Printing