TPSF yahamasisha vijana kulima mboga na matunda kibiashara

Mmoja wa vijana walioamua kujiajiri kupitia sekta ya kilimo cha mboga na matunda akifanya kumwagilia shamba lake la vitunguu katika eneo la mazombe Wilayani Kilolo Mkoa wa Iringa. Changamoto kubwa inayomkabili ni kukosa mtaji wa kuendelea na shughuli hiyo ambayo inamuigiza kipato cha kujikimu kimaisha.


Mmoja wa vijana walioamua kujiajiri kupitia sekta ya kilimo cha mboga na matunda akifanya kumwagilia shamba lake la vitunguu katika eneo la mazombe Wilayani Kilolo Mkoa wa Iringa. Changamoto kubwa inayomkabili ni kukosa mtaji wa kuendelea na shughuli hiyo ambayo inamuigiza kipato cha kujikimu kimaisha.

Na Moses Mahundi, Kilolo

Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Sekta Binafsi Nchini (TPSF) Bi.Angelina Ngalula, amesema jana hapa  kwa kuwa  mboga na matunda vina soko la uhakika ndani na nje ya Tanzania, vijana wakilima mazao haya watajiajiri haraka na kushinda umaskini kwa kiasi kikubwa.
 Akiongea na wakulima wadogo baada ya kuvutiwa na mashamba yao ya mboga na matunda katika Kijiji cha Mazombe. Wilaya ya Kilolo, Mkoa wa Iringa na pia kusikiliza changamoto wanazowakabili, Mwenyekiti huyo amewataka vijana wa Tanzania kulilma mboga na matunda na kutokana na adha ya umasikini.
“Mboga na matunda vina soko kubwa sana nje ya nchi hususani nchi za Ulaya. Jukumu letu kuzalisha na  kupeleka mzigo mingi nje ya nchi na kuleta fedha ya kigeni nchini,” amesema Bi.Ngalula na kuwaomba vijana wajiingize katika kilimo hicho.
Bi Ngalula amesema moja ya changamoto kubwa nchini ni  kilimo  chamazoea ambacho kinatoa mazao yasiyokidhi  ubora  soko. “Tuna jukumu la kupeleka elimu ya kilimo bora cha mboga na matunda kwa wakulima wetu kote nchini ili   uzalishaji uwe na tija na mazao yaongezeke,” amesema.
Amewapongeza wakulima wa Mazombe na kuahidi kuwapeleka Mazombe wataalum kutoka Chama cha Wakulima wa Mboga na Matunda Tanzania (TAHA) ili wawape ujuzi unaotakiwa na kuinua kipato chao.
“Niwaomba  vijana, hase wanawake, mjiunge katika vikundi  ili muweze kufikiwa  kwa urahisi na watoa huduma mbali mbali,  ikiwa ni pamoja na taasisi za kifedha zinazoweza kuwapa  mikopo,” amesema Bi.Ngalula.

“Serikali inaendelea kutekeleza wajibu wake na kushirikiana na sekta binafsi. Hatua hizo  ni pamoja na kuhakikisha biashara zinafanyika kwa urahisi na serikali inapata mapato yake na wafanyabiashara wananufaika na shughuli zao.”
Mwenyekiti wa kikundi hicho, Bw.Hassan Ally Kikoti, ameomba  TPSF iwaunganishe na taasisi za kifedha ili  kukopeshwe na kuendelea kilimo chao.
“Changamoto kubwa tuliyonayo ni mitaji ya kuendeleza kilimo cha mboga. Kwa kukosa fedha tunazalisha kidogo kuliko mahitaji ya soko,” amesema Bw.Kikoti
Mmoja wa wakulima, Bw Alex Msumile, amesema kilimo kweli kinatoa ajira lakini akaongeza kwamba wanakabiliwa  upatikanaji wa masoko ya uhakika na bei nzuri kwa mazao yao. jambo ambalo limekuwa likiwarudisha nyuma kimaendeleo.
“Niwaomba vijana wenzangu tuelekeze nguvu kwenye kilimo.  Hii ni sekta yenye kumpa  mtu ajira na kipato,” amesema Bw Msumile.

Comments

Popular posts from this blog

Mbeya agro-processors get 5 acres to build 50 industries

Tanzania praised for being keen on fertilisers going to farmers

Gold mine in Songwe wins ministerial praise for protecting environment