Majaliwa asifu wajenzi wa kiwanda cha sukari Bagamoyo

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo(TADB)Bw.Japhet Justine akitoa maelezo kwa Waziri Mkuu Mkuu Kassim Majaliwa namna Benki hiyo ilivyoshiriki katika uwezeshaji wa ujenzi wa kiwanda cha Sukari Bagamoyo(BSL) alipotembelea kujionea hatua iliyofikiwa ya ujenzi wa kiwanda hicho Kilichopo Wilaya ya Bagamoyo ,Mkoani Pwani jana.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa(watatu kushoto) akiwa katika ziara yake Wilayani Bagamoyo Mkoa wa Pwani kukagua hatua iliyofikiwa ya ujenzi wa Kiwanda cha Sukari (BSL) ambapo kukamilika kwa ujenzi wa kiwanda hicho kutasaidia kupunguza changamoto ya upatikani wa Sukari hapa nchini. Wapili  kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Kilimo Tanzania(TADB) Bw.Japhet Justine.



Na Abdallah Luambano, Bagamoyo

Waziri Mkuuu Kassim Majaliwa  amesifu wajenzi wa Kiwanda cha Bagamoyo (BSL) kinachofadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB) kwa shilingi bilioni 15 na kusema kukamilika kwa kiwanda hicho  kutapungaza uagizaji wa sukari kutoka nje.

Akizungumza na wageni na wafanyakazi wa kiwanda hicho jana, Waziri Mkuu  amesifu ujenzi wa kiwanda hicho na kusema:

“Mahitaji ya sukari ya mezani kwa sasa hapa nchini ni tani 450,000 ,  uzalishaji wetu ni tani 380,000.  Tuna upungufu wa tani 70,000. Niwapongeze wawekezaji wanaojenga kiwanda hiki  na taasisi zote za fedha kwa jitihada zilizochukuliwa mpaka kujengwa kwa kiwanda hiki.  Kiwanda  kikianza kufanyakazi tutaweza kukidhi  mahitaji ya yetu ya ndani,’’ amesema Waziri Mkuu.

Waziri Mkuu amewataka Watanzania kubadilika na kuanza kujivunia bidhaa zinazozalishwa  nchini na kutokana na kasumba ya kuamini bidhaa za nje ni nzuri zaidi.

“Rais wetu Dk. John Pombe Magufuli huwa anasema tunaweza na leo nimethibitisha pasipo na mashaka yoyote kwamba Watanzania tunao uwezo wa kifedha kufanya uwekezaji, wataalamu wa kuendesha mitambo na hata usimamiaji wa miradi mikubwa, tujivunie hilo,’’ amesema.

Mkurugenzi wa Makampuni ya Bakhresa, Bw. Abubakar Bakhresa,  mbali ya kumshukuru Rais Magufuli kwa kuwapatia shamba  lenye hekta 10,000, ambalo watalitumia kuzalisha miwa na ameahidi  kuendelea kuunga mkono jitihada za serikali za kuipeleka nchi kwenye uchumi wa viwanda.

“Tunamshuru Rais Magufuli kwa kutupatia eneo hili ambalo  tutalitumia kuzalishamiwa kama malighafi ya kiwanda. Jambo muhimu zaidi kwetu ni kuendelea kuunga juhudi za serikali za kujenga uchumi wa viwanda ifikapo 2025,’’ amesema.

Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Japhet Justine,  amesema mbali ya kuwezesha kiwanda hicho, Benki imelenga pia kuwanufaisha wakulima wadogo wa miwa.

“Kwa kawaida wenye mabenki hawawezi kumkopesha mkulima bila kuliona eneo. Sisi tumeona fursa.  Fursa hiyo ni kwamba awamu ya pili ni kuhakikisha uzalishaji unakuwa endelevu.  Katika fursa hii na awamu hii tutawakopesha wakulima wadogo kwa masharti nafuu ili waendeleze mashamba yao,’’ amehadi Bw. Justine.

Mkurugenzi wa Mahusiano wa Makampuni ya Bakhresa, Bw. Hussein Sufian, amesema gharama za mradi ni Dola za Marekani milioni 100 ambapo TADB imetoa Dola za Marekani milioni 6.5 sawa na shilingi za bilioni 15.  

Mabenki mengine ni  CRDB Bank ambayo imetoa dola milioni 25, Standard Chartered imetoa dola milioni 10 na dola milioni 30 zimetolewa na makampuni ya Bakhresa na kufikisha asilimia 70 ya mtaji wa mradi wa ujenzi wa kiwanda.


Comments

Popular posts from this blog

Gold mine in Songwe wins ministerial praise for protecting environment

Tanzania praised for being keen on fertilisers going to farmers

Kirenga: Kipaumbele chetu ni mkulima mdogo kupata soko la uhakika