Dampo la Nsalaga Uyole hatari kwa afya za watu na mazingira, aonya Suma

-->
NAIBU Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Bw. Mussa Sima wa pili kushoto  akizungumza mara baada ya kutembelea  eneo Mfereji wa umwagiliaji wa mnazi, uliopo wilaya mbalali ambao utumika katika skimu za kilimo cha zao la Mpunga. Wakati wa ziara yake  ya kikazi kukagua uzingatiaji wa  Sheria ya Mazingira katika mikoa ya nyanda za juu kusini.  Kulia ni Mwenyekiti wa Baraza  la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira nchini (NEMC),Prof. Esnati Chaggu  kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dkt. Samuel Gwamaka, katikati ni Mkuu wa Hifadhi ya   Taifa ya Ruaha  Bw. Izumbe Msindai (SACC) na wapili  ni Mkuu wa Wilaya ya Mbalali Bw. Reuben Mfune.
-->
NAIBU Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Bw. Mussa Sima wa pili kushoto  akipewa maelezo na Mkuu wa hifadhi  ya Taifa  ya Ruaha Bw Izumbe  Msindai (SACC) Wakati alipotembelea   eneo Mfereji wa umwagiliaji wa mnazi, uliopo  wilayani mbalali   unaopakana na Hifadhi ya Taifa ya Ruaha ambao utumika katika skimu za kilimo cha zao la Mpunga. Wakati wa ziara yake  ya kikazi kukagua uzingatiaji wa  Sheria ya Mazingira katika mikoa ya nyanda za juu kusini.  Wa pili  Kulia ni Mwenyekiti wa Baraza  la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira nchini (NEMC),Prof. Esnati Chaggu, kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dkt. Samuel Gwamaka, Na wa tatu kulia ni  ni  Mkuu wa Wilaya ya Mbalali Bw. Reuben Mfune.

-->
NAIBU Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Bw. Mussa Sima  kushoto  akipewa maelezo na Mkuu wa hifadhi  ya Taifa  ya Ruaha Bw Izumbe  Msindai (SACC) wa pili kushoto Wakati alipotembelea   eneo Mfereji wa umwagiliaji wa mnazi, uliopo  wilayani mbalali   unaopakana na Hifadhi ya Taifa ya Ruaha ambao utumika katika skimu za kilimo cha zao la Mpunga. Wakati wa ziara yake  ya kikazi kukagua uzingatiaji wa  Sheria ya Mazingira katika mikoa ya nyanda za juu kusini.   Kulia ni Mwenyekiti wa Baraza  la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira nchini (NEMC),Prof. Esnati Chaggu, Wa pili kulia  ni Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dkt. Samuel Gwamaka,  Na wa tatu kulia ni  ni  Mkuu wa Wilaya ya Mbalali Bw. Reuben Mfune.


Na Isdory Njavike, Uyole

Naibu  Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Bw. Mussa Sima,  ameghadhabishwa na ujenzi duni wa dampo la taka la Nsalaga Uyole, Mkoani Mbeya, na kuonya kwamba miundombinu hni hatari kwa afya za watu na mazingira kwa ujumla.

Amelitaka Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira nchini (NEMC) kushirikiana na ofisi za Mkoa wa Mbeya ili kupata ufumbuzi wa tatizo hilo kwani dampo limejengwa bila kuzingatia kanuni za kuhifadhi mazingira na pia utupaji taka kwenye dampo umekuwa ukirudidha uchafu kwenye makazi ya watu.  Taarifa alizopata ni kwamba dampo limejengwa bila utafiti wa kitaalamu wa kutosha.

Akizungumza mara baada ya kutembelea  eneo la Nsalaga Uyole, katika   ziara yake  ya kikazi kukagua uzingatiaji wa  Sheria ya Mazingira. katika mikoa ya nyanda za juu kusini, amekumbusha kwamba  taka lazima zitenganishwe kwenye vyanzo kabla ya kuingizwa kwenye dampo.

“Kuanzia sasa watafutaji taka wasiruhusiwe kuingia kwenye mashimo ya dampo kwani wamekuwa wakirudisha uchafu kwenye makazi ya watu na kuchafua mazingira,” amesema naibu waziri huyo.

Bw. Sima ambaye ameambatana  na  na Mwenyekiti wa  Bodi ya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira nchini (NEMC),Profesa Esnati Chaggu, Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dk. Samuel Gwamaka pamoja na  maafisa  wengine wa NEMC, amewataka wasimamizi wa dampo hilo kujifunza kutoka kwa wasimamizi wa madampo katika mikoa mingine ambako  madampo ya kisasa tayari yamejengwa na yanahifadhi  mazingira.

“Halmashauri ya Mkoa wa Mbeya  mjipange na kuhakikisha mnatenga eneo maalum ya shughuli za urejelezaji ili kuondoa  mlundikano wa  uchafu, kwani mmekuwa mkichanganya uchafu na taka ngumu ambazo ni ngumu kuzizoa,” ameagiza naibu waziri huyo.

 Prof. Chaggu amesema majitaka yatokayo katika dampo (leach ate) yana sumu kiasi kikubwa na kufafanua kwamba majitaka hayo yana asilimia 8 juu ya majitaka yatokayo majumbani. Ametaka majitaka hayo yasimamiwe kwa umakini ili yasitiririke katika mazingira na kudhuru jamii inayoishi karibu na dampo hasa katika kipindi cha mvua.

 Prof. Chaggu amesema utunzaji wa mazingira unapozingatiwa,  mazingira yanakuwa salama na afya za Watanzania zinaboreka na uchumi unakua.

Dk Gwamaka amefafanua kwamba kwa mujibu was  Sheria ya Mazingira na Kanuni za Usimamizi wa Taka ngumu, halmashauri za wilaya zina wajibu wa kutenganisha taka na kuelimisha wananchi jinsi ya kufanya hivyo.
  
“Sheria  ya Mazingira ya Mwaka 2004,  kuna Kanuni za Usimamizi wa Taka ngumu ambazo zimeeleza kwa mapana  wajibu wa halmashauri za wilaya juu ya kutenganisha taka na kuelimisha wananchi jinsi ya kufanya hivyo. Wakati ni huu wa kutekeleza maagizo hayo  kwa kuanza kutoa elimu. Tutashirikiana kwa karibu na halmashauri kuhakikisha tunalitimiza hilo”. ameahidi Dk. Gwamaka.

Amefafanua  kuwa taka ni fursa na kutoa mifano kwamba  taka za glasi na plastiki zinaaweza kuwa  malighafi kwenye viwanda vya urejelezaji na kukuza uchumi kwani viwanda vinalipa kodi kwa serikali.






Comments

Popular posts from this blog

Mbeya agro-processors get 5 acres to build 50 industries

Tanzania praised for being keen on fertilisers going to farmers

Mavunde: TADB offered 1.8bn/- to nurture Farm Access