Chuo cha Diplomasia chaanzisha kosi ya diplomasia ya uchumi kuchochea viwanda

Kaimu Mkurugenzi  wa kituo  cha Diplomasia na uhusiano wa Kimataifa(CFR), Dkt.Jeremia Ponera  kulia akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari ofisini kwake jana  Jijini Dar es salaam, kuhusu  namna kituo hicho kilivyoboresha   huduma zake kwakuanzisha  kozi pamoja na programu maalumu za diplomasia sambamba na kuandaa wataalamu watakao wakilisha  vema Tanzania nje ya nchi, kushoto ni Msajili wa kituo hicho Dkt.Ally Masabo.

Msajili wa kituo  cha Diplomasia  na Uhusiano wa Kimataifa (CFR), Dkt. Ally Masabo, kushoto akikagua eneo la mradi  wa ujenzi wa maktaba ya kisasa,hosteli na vyumba vya semina na kufundishia  unaendelea kituoni hapo,  ambapo mpaka sasa serikali imeshatoa takribani shilingi bilioni 12 kwaajili ya ujenzi huo,  Kulia  ni Mhandisi,Athuman Mashaka.



Na Abdallah Luambano, Dar es Salaam

CHUO  cha Diplomasia na Uhusiano wa Kimataifa (CFR) cha Jijini Dar es Salaam, kimeanzisha kozi ya diplomasia ya uchumi kwa wahitimu wa vyuo vikuu ili kunyanyua na kuimarisha  uwezo wa majadiliano katika masuala ya uchumi, hasa ya kimataifa,  wa wafanyakazi katika balozi za Tanzania na watendaji katika  sekta binafsi.

Akizungumza na waandishi wa habari  jijini hapa jana, Kaimu Mkurugenzi wa chuo hicho, Dkt. Jeremia Ponera, amesema mafunzo haya yanaandaa wataalamu wa Tanzania kushiriki  vizuri na kikamilifu katika  utekelezaji wa  azma ya taifa ya kujenga uchumi wa kati na wa viwanda ifikapo 2025.

“Kituo hiki, kama taasisi nyingine  za umma, tumekuwa mstari wa mbele katika kutafsiri na kuunga mkono jitihada za serikali. Katika kipindi hiki ambacho serikali imeazimia kujenga uchumi wa viwanda ifikapo 2025, kituo kinawaandaa wataalamu ambao watasaidia kueleza fursa zilizopo kimataifa ili kufikia azma hiyo kwa haraka,’’ amesema Dkt. Ponera.

Amesema Chuo hicho kimeisaidia Tanzania kuwaandaa mabalozi, wafanyabiashara za kimataifa katika kutambua fursa na kufanya  majadiliano yenye tija kwa taifa.  Chuo pia kimewasaidi mabalozi na wafanyabiashara kutambua umuhumu wa  uwekezaji na kueleza fursa zilizopo Tanzania.

"Kama taasisi tupo katika nafasi nzuri ya kufanikisha azma ya Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli ya kuleta mageuzi katika ujenzi wa uchumi wa kati na viwanda," alisema Dkt. Ponera na kuongeza kuwa kila mtanzania anapaswa kuunga mkono juhudi hizo kwa vitendo.

“Mbali ya kujikita katika kutafsiri malengo ya serikali kulingana na nyakati zilizopo, Chuo kimefanya kazi kubwa katika kuwaandaa Mabalozi ambao ni wawakilishi muhimu kimataifa. Lakini pia tumekuwa na kozi fupi za kuwaandaa wafanyabiashara za kimataifa pamoja na kuonesha fursa zilizopo kwa wawekezaji wa kigeni hapa nchini,’’ ameeleza.

Aidha amesema  kuwa chuo kimetengeneza programu mpya zinazojielekeza katika ujenzi wa uchumi wilayani na mikoani ili kuchochea ukuaji wa uchumi wa ndani na hivyo kufikiwa kwa azma ya uchumi wa viwanda.

“Chuo hakijishughulishi tu na masuala ya kimataifa, bali hata ndani ya nchi ambapo programu mbalimbali zinazojielekeza katika ujenzi wa uchumi kwenye maeneo ya wilaya na mikoa kwa kuwa diplomasia ya uchumi inahusu namna ya kuongeza biashara za ndani na nje na kuangazia maeneo muhimu ya kiuwekezaji,’’ alieleza

 Msajili wa Chuo,  Dkt. Ally Masabo, ametoa wito kwa Watanzania kujiunga na chuo hicho hasa katika kipindi hiki ambacho diplomasia ya uchumi imekuwa dhana muhimu katika kujenga chumi za mataifa mbali mbali.

“Chuo cha Diplomasia kinatoa kozi za muda mfupi na muda mrefu ambazo zimejikita katika kuwajenga Watanzania kujua fursa zilizopo kimataifa ili wazitumie katika kuchochea maendeleo ya ndani ya nchi.  Natoa wito kwa Watanzania kujiunga na chuo hiki,’’ amesema na kuongeza kuwa sifa za waombaji ni kuanzia wahitimu wa darasa la saba, wahitimu wa cheti, kidato cha nne na kidato cha sita.

Chuo cha Diplomasia kimeanzishwa mwaka 1978 na kinaendeshwa kwa ubia baina ya serikali ya Tanzania na Msumbiji.  Chuo kina  jukumu la kutoa mafunzo ya diplomasia, stretejia pamoja na lugha.


Comments

Popular posts from this blog

Mbeya agro-processors get 5 acres to build 50 industries

Tanzania praised for being keen on fertilisers going to farmers

Mavunde: TADB offered 1.8bn/- to nurture Farm Access