Msimwage majitaka katika mitaro ya mvua, NEMC yaonya wakazi wa mijini
Na Mosses Fedirnand, Dar es
Salaam
Baraza la Taifa la Hifadhi na
Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limewataka Watanzania,hasa waishio mijini,
kuacha kabisa kutiririsha majitaka katika mitaro iliyojengwa kusafirisha
maji ya mvua kwani tabia hiyo inahatarisha afya ya umma na kuharibu mazingira.
Akiongea jana baada ya kutembelea
eneo la makazi la Mabibo na Ukanda Maalumu wa Viwanda katika eneo hilo, Jijini
Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dk Samuel Gwamaka, amesema ameshtushwa
kuona wananchi wameelekeza mabomba ya majitaka kutoka majumbani mwao na
kumwaga majitaka hayo katika mtaro mkubwa wa umma unaosafirisha
maji ya mvua hadi Mto Msimbazi na kwenda baharini. NEMC imekuwa ikikemea
tabia hiyo mara kwa mara.
Amesema
jambo hilo limemsikitisha sana na kufafanua kwamba kasoro hiyo
inahatarisha afya ya wananchi wa Mabibo na wa mbali na kuharibu mazingira.
“Wananchi kuelekeza mabomba ya majitaka kwenye mitaro maalumu ya umma
siyo matumizi sahihi ya mitaro hiyo ya umma.
Tunawaonya wananchi wanaofanya
hivyo nchini kuacha mara moja tabia hiyo kwani inahatarisha afya ya umma na
kuaharibu mazingira,” ameeleza. Dk Gwamaka ametembelea eneo la Mabibo baada ya
NEMC kupokea barua inayolalamikia kiwanda cha kutengeneza nguo kwa uchafuzi wa
mazingira kwa njia ya moshi, kelele na maji yenye kemikali na sumu.
“Jambo hili litafuatiliwa kwa makini kwa kuunda timu ya wataalaamu.
Ikibainika kwamba kiwanda chochote kimekiuka matakwa ya Sheria ya Mazingira ya
2004, hatua kali za kisheria zitachukuliwa,” ameeleza.
Hata hivyo Dk Gwamaka amewataka
wananchi kuacha tabia ya kunyoshea vidole taasisi au kiwanda huku wao wakiwa
mstari wa mbele katika kuharibu mazingira badala ya kuyalinda.
Mtaalamu huyo amewataka wananchi na viongozi kuelewa kwamba mazingira salama ni muhimu kwa ustawi wa watu, wanyama na viumbe vingine na kuwaomba viongozi wa serikali za mitaa kuhakikisha miundombinu inatumika kwa shughuli tu liliyokusudiwa. “Mamlaka zote tukisimamia hili tutaepusha madhara kwa wananchi, mifugo na viumbe vingine vilivyomo katika mazingira yetu,”ameeleza.
Mtaalamu huyo amewataka wananchi na viongozi kuelewa kwamba mazingira salama ni muhimu kwa ustawi wa watu, wanyama na viumbe vingine na kuwaomba viongozi wa serikali za mitaa kuhakikisha miundombinu inatumika kwa shughuli tu liliyokusudiwa. “Mamlaka zote tukisimamia hili tutaepusha madhara kwa wananchi, mifugo na viumbe vingine vilivyomo katika mazingira yetu,”ameeleza.
Dr Gwamaka amewataka Watanzania
kuyalinda mazingira wakielewa kwamba ustawi wa wao na shughuli nyingine
zote zinategea usalama wa mazingira ya Tanzania. Hakusema ni lini timu ya
wataalamu itaanza kazi yake lakini amedokeza kuwa timu itaanza kazi yake baada
ya muda mfupi ujao.
Comments
Post a Comment