Wajasiriamali wanawake waelezwa fursa zilizopo Comoro
Na Daniel Lwimiko, Dar es Salaam
NAIBU Balozi wa Comoro nchini Tanzania, Balozi Bacar Salim,
ameuambia mkutano wa maandilizi ya Maonyesho ya Bidhaa za Tanzania yanayotarajiwa kufanyika Comoro katikati ya mwezi kesho kwamba washiriki wapeleke Comoro bidhaa za chakula, viungo, dawa za asili, asali, dagaa pamoja na bidhaa za viwandani, hasa samani za ndani.
Mkutano huo umeitishwa na Mfuko wa Saccos wa Wajasiriamali Tanzania
(TASWE) au Tanzania Saccos for Women Entrepreneurs kuwaandaa wajasiriamali watakoshiriki katika maonyesho ya siku nane yanayotaratijiwa kufunguliwa na Rais wa Comoro, Aprili 17 na kufungwa Aprili 24, mwaka huu. Maonyesho hayo yatavuma kama Wajasiriamali Wanawake wa Tanzania Tumekuja Comoro.
“Jambo muhimu kwenu ni kujua bidhaa ambazo Wakomoro wanazihitaji. Kwa
muda mrefu tumekuwa tukiagiza bidhaa za chakula, viungo, dawa za asili, asali, dagaa pamoja na bidhaa za viwandani kutoka nchi mbalimbali. Hivyo wakati mkijiandaa na ziara hiyo ya kibiashara ni vyema mkaangalia hayo maeneo,’’ ameshauri Balozi Salim.
Naibu balozi huyo amepongeza jitihada za akina mama ambazo
amesema
zinaimarisha uhusiano wa muda mrefu kati ya Tanzania na Comoro.
Amesema watu wa nchi hizo mbili wamekuwa wakifanyabiashara
kwa muda
mrefu. “Hivyo ni jukumu letu kuweka mazingira mazuri na ambayo ni endelevu kwa manufaa ya vizazi vya leo na kesho.’’ Mwenyekiti wa TASWE, Bi Anna J. Matinde amesema kuwa maandalizi yote ya safari hiyo yamekamilika.
“Kwa kiasi kikubwa maandalizi ya safari yamekamilika. Kwa sasa
tunaangalia mambo machache ikiwemo viza. Makadirio yetu yalikuwa tuondoke na wajumbe 60 lakini mkutano huu umeongeza hamasa kwani wajumbe wengine wamejitokeza na hivyo kuongeza idadi ya washiriki,’’ ameeleza Bi Matinde, na kuwapongeza wajumbe kwa kuhudhuria mkutano huo ambao amesema umewapa nafasi ya kufahamu fursa za biashara zilizopo nchini Comoro.
“Tumekuwa tunapata shida kueleza fursa zinazopatikana nje ya
mipaka
yetu. Lakini kuwepo kwa ujumbe mzito kutoka Ubalozi wa Comoro hapa nchini kumerahisisha kufikisha ujumbe na Watanzania wamesikia. Tunaamini kuwa maonyesho haya yatakuwa ya mafanikio makubwa,’’ alisema.
Meneja wa TASWE, Bi Lilian Nyagabona, ambaye anasimamia
iitifaki,
ameeleza kuwa maonyesho hayo yanayotarajiwa kufunguliwa na Rais wa
Comoro. “Haya yatakuwa ni maonyesho yenye mvuto wa aina yake kwani serikali za nchi zote mbili wameyabariki na tutaondoka hapa. Taarifa tulizonazo ni kwamba yatahudhuriwa na watu wengi wakiwemo wafanyabiashara na wakezaji wa huko Comoro,’’ ameeleza Bi. Nyagabona. Mwisho.
|
Comments
Post a Comment