Na
Moses Ferdinand, Dar es salaam
Benki
ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania(TADB) kwa kushirikiana na Wakala wa Taifa wa
Uhifadhi wa Chakula(NFRA) wameingia makubaliano kuongeza thamani ya mnyororo wa thamani wa zao la mahindi kwa
kuhakikisha wakulima wa zao hilo hapa
nchini wanapata soko la uhakika ili waweze kunufaika na shughuli ya kilimo.
Akizungumza
na waandishi wa habari mara baada ya kumaliza kikao cha pamoja,
Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Japhet Justine alisema wamekubaliana na NFRA kuhakikisha zao la mahindi
linapata soko jambo litakalompa uhakika
mkulima kuendelea na kilimo cha zao hilo.
“TADB
ilishatoa zaidi ya bilioni 3.4 kwa vikundi 22 vya wakulima katika kufanya
kilimo cha kisasa cha zao la mahindi, hivyo kupitia kikao hiki tunawahakikishia wakulima wa mahindi
soko la uhakika,” alisema Bw.Justine
Alisema
kwa msimu wa kilimo uliopita soko la zao la mahindi liliyumba hivyo kupitia
mazungumzo kati ya TADB na NFRA yataibua matumaini kwa wakulima wengi wa mahindi kwa kupata soko la bidhaa
hiyo ambayo bei yake ilishuka kutokana na
uzalishaji kuongezeka tofauti na mahitaji ya nchi.
“Pamoja na Shirika la Chakula Duniani(WFP)
kununua zaidi ya tani 36,000 za mahindi
bado shehena nyingi za mahindi zipo kwa wakulima, hivyo kama wadau wa sekta ya kilimo ni wajibu wetu
kuhakikisha shehena hizo zinapata soko,”
alisema .
Hivi
karibuni, Rais John Pombe Magufuli alishuhudia utiliaji wa makubaliano
Ikulu Jijini Dar es Salaam kati Serikali kupitia Wizara ya Kilimo na WFP kuhusu kununua kiwango kikubwa cha
mahindi.
Bw.Justine
alisisitiza kuwa ili kumfanya mkulima kuendelea na kilimo cha zao hilo
ni lazima ahahakikishiwe soko la bidhaa yake itakayompa hamasa ya kulima kwa tija ili aweze kupata mavuno kwa
wingi na tija inayotakiwa sokoni.
“TADB
itaanda mkakati wa pamoja na NFRA utakaoleta mabadiliko makubwa katika
mnyororo wa thamanai wa zao la mahindi nchini, hii ni kutokana ana changamoto mbalimbali zilizojitokeza katika msimu
wa kilimo uliopita ulifanya zao la
mahindi kushuka thamani,” alisema Bw.Justine
Aliongezea
kuwa kupitia mikataba wanayoingia NFRA na wanunuzi kutoka nje ya nchi
itatupa mwongozo wa kuhamasisha kilimo nchini kwa kuwakopesha wakulima kupitia Mfuko wa Dhamana kwa
Wakulima wadogo(SCGS) katika kufanya
kilimo chenye tija na kukidhi mahitaji ya soko.
Alisema
lengo letu ni kuhakikisha bei ya zao hili sokoni inakuwa ya kumnufaisha
mkulima kwa kipindi chote cha msimu hali itakayomfanya mkulima kurudisha fedha yake na kupata faida
itakayompelekea kufanya maendeleo.
“Serikali
ya Awamu ya Tano Chini ya Rais Dkt.John Magufuli imejipambanua kuboresha
mazingira ya wananchi wa hali ya chini wakiwemo
wakulima, hivyo TADB kwa nafasi yetu tunaendelea kutekeleza azma ya Serikali kwa kuboresha mazingira kwa wakulima
nchini,” alisema Bw.Justine
kwa
upande wake Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa NFRA Bi.Vumilia Zikankuba alisema
wamefanya mazungumzo mazuri na TADB ambayo yatawasaidia kama wakala katika kutekeleza majukumu yake ya kuhakikisha
zao la mahindi linapata soko.
“NFRA
imejipanga kupunguza utegemezi kwa Serikali katika kufanya shughuli zake, hivyo
tunashirikiana na wadau wa kilimo na Taasisi za kifedha kama TADB kutuwezesha
fedha zitakazo tusaidia kuendesha shughuli zetu za uhifadhi wa mazao na kujenga
masoko,” alisema Bi.Zikankuba
Alisema
kupitia mazungumzo yetu tunauhakika wa kupata fedha zitakazo kuwezesha
kununua mahindi kutoka kwa wakulima hivyo kutoa uhakika kwa mkulima kuwa soko la zao hili lipo na kama wakala
tutajitahidi kuhakikisha tatizo la
ukosefu wa soko unapungua au kuisha kabisa.
Wakulima
wa Mikoa ya Nyanda za juu Kusini ikiwemo Ruvuma,Rukwa wamekuwa
wakilalamikia soko la mahindi hivyo kuiomba Serikali kuisaidia kupata soko la uhakika kwa ajili ya zao hilo
ili kuweza kumudu bei za pembejeo
za kilimo.
Mwisho.
Comments
Post a Comment