Bashungwa avutiwa na kazi za SAGCOT
Na
Jackson Kulinga, Dar es salaam
NAIBU
Waziri wa Kilimo, Bw. Innocent Bashungwa amepongeza kazi inayofanywa na
Kituo cha Kuendeleza Kilimo Nyanda za Juu Kusini(SAGCOT)
kwa kuweza kuwafikia wakulima wengi katika ukanda huo na kufanya mageuzi kwenye sekta ya kilimo kwa kuongeza
tija katika uzalishaji.
Akizungumza
katika ziara yake ya kwanza alipotembelea Kituo hicho jijini Dar es
salaam mwishoni mwa wiki ilikujionea utendaji kazi wake, naibu waziri Bashungwa alisema amefurahishwa na
kazi zinazofanywa na kituo hicho
ikiwemo kuwaunganisha wakulima na kuwajengea
uwezo na mbinu za kilimo biashara.
“Ziara
yangu katika ofisi yenu imekuja mara baada ya kuona kazi nzuri na ushuhuda
mbalimbali kutoka kwa wakulima katika mikoa ya Njombe na Iringa hivyo ikanisukuma niwatembelee ili
tufahamiane na kujifunza kazi zenu,”
alisemaBw. Bashungwa.
Alisema
utendaji kazi wa SAGCOT umeleta matokeo chanya kwa wakulima katika mikoa
ya nyanda za juu kusini hivyo ni muhimu kwa wadau mbalimbali wa kilimo kote nchini kujifunza kupitia
mfumo unaotumiwa na SAGCOT ili
kuleta mageuzi katika sekta ya kilimo.
“Uzalishaji
umeogezeka katika maeneo ambayo SAGCOT inafanya kazi na wakulima. Hii
imepelekea uchumi kwa wakulima kuimarika kutokana na uhakika wa uzalishaji na masoko ambapo SAGCOT ndiyo
muunganishi,” alisema.
Alisema
kwa kufuata mfumo huu wa SAGCOT, utekelezaji wa Mpango wa Awamu ya
Pili wa Kuendeleza Sekta ya Kilimo (ASDP II) utakuwa wa mafanikio kwani njia nzuri imeonyeshwa kupitima maeneo
ambayoyo SAGCOT inafanya kazi zake.
“Wakulima
wa chai mkoani Njombe wamefaidia kwa kilimo cha chai kupitia washirika wa
SAGCOT ambao ni Kampuni ya kuhudumia wakulima wadogo Njombe(NOSC), hii inaonesha ni kwa namna gani SAGCOT
imejipanga kuleta mapinduzi ya kilimo
nchini,” alisema Naibu Waziri Bashungwa.
Aidha
Naibu Waziri huyo aliagiza NOSC kueneza utaalum wa kuendeleza zao la chai
katika mikoa mingine ili kuliendeleza kwani ardhi nzuri ya kilimo cha zao hilo ipo katika maeneo mbali mbali hapa
nchini hivyo ni jukumu la wadau katika
kuendeleza.
“Serikali
itaendelea kushirikiana na SAGCOT na wadau mbalimbali katika jitihada za
kukuza na kuendeleza sekta ya kilimo kwa kuzalisha malighafi kwa tija ambayo ndiyo chachu ya
uanzishwaji wa viwanda,” alisema
Alisema
kwa kushirikiana kwa pamoja tutaweza kutekeleza ASDP II kwa muda
uliopangwa na pia kufanya azma ya Serikali ya kufikia uchumi wa kati na viwanda ifikapo mwaka 2025 kufikiwa kwa
vitendo kwani njia ya kuelekea katika
mafanikio imeshaanza kupitia SAGCOT.
“Niwaombe
SAGCOT kuwashirikisha vijana wajikite katika sekta ya kilimo kwani ndiyo
kwenye uhakika mkubwa ajira , hivyo ni muhimu vijana wakahusishwa zaidi ili kupunguza wimbi la vijana
kukosa ajira na badala yake wakajikita
zaidi kwenye sekta ya kilimo,” alisema Naibu Waziri Bashungwa
Kwa
upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa SAGCOT,Bw.Geoffrey Kirenga alishukuru
ujio wa Naibu waziri huyo na taarifa ya utendaji kazi wa Kituo na mipango ya kufanya mageuzi katika sekta
ya kilimo nchini kwa kuanza na ukanda wa
nyanda za juu kusini.
“Ujio
wa mheshimiwa naibu wazirin umekuwa ni faraja kwetu kwani ameweza
kufahamu dhumuni la kituo chetu na zaidi ameweza kutoa mapendekezo na maagizo ambayo kama SAGCOT tumeyapokea
na tutakwenda kuyatekeleza kikamilifu,”
alisema Bw.Kirenga.
Alisema
mapendekezo yake yote yatafanyiwa kazi lengo likuwa kuboresha huduma katika
kukuza na kuendeleza kilimo nchini kwa kumwinua mkulima mdogo kwa kushirikana na wadau na watoa huduma
mbalimbali za kilimo.
SAGCOT
ambayo imefanikiwa kuwaunganisha wakulima wadogo na kuwajengea
uwezo kupitia mafunzo mbalimbali imeshazindua kongani tatu mpaka sasa ambazo ni Ihemi inayoshughulikia mikoa ya Iringa na Njombe, Kongani ya Mbarali kwa mikoa ya Mbeya na Songwe na pia kongani ya Kilombero kwa Mkoa wa Morogoro na wilaya zake zote.
uwezo kupitia mafunzo mbalimbali imeshazindua kongani tatu mpaka sasa ambazo ni Ihemi inayoshughulikia mikoa ya Iringa na Njombe, Kongani ya Mbarali kwa mikoa ya Mbeya na Songwe na pia kongani ya Kilombero kwa Mkoa wa Morogoro na wilaya zake zote.
Mwisho.
Comments
Post a Comment