Buchafwe ahimizwa kusoma vitabu kuongeza maarifa



Na Moses Mahundi, Dar es Sala

Watanzania, hususani vijana,  wametakiwa  kujenga utamaduni wa kusoma vitabu ili waweze kupata na kuongeza maarifa ili waweze kufikia ndoto zao katika maisha.
Wito huo umetolewa na  na mwandishi wa kitabu cha “Talk to God” (Ongea na Mola),  Bw. Masija Buchafwe,  alipoongea na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam jana wakati akitambulisha kitabu hicho.

“Ndani ya vitabu kuna maarifa mengi ambayo ni msaada mkubwa kwa watu wa rika mbali mbali katika kukabiliana na changamoto za maisha za kila siku, hivyo itakuwa ni jambo muhimu sana kama taifa watu wake wakawa na utamaduni wa kujisomea vitabu.  Mimi naweza kuzungumzia Tanzania. Kwa maoni yangu toafauti na miaka ya 1950 hadi  1970 Tanzania ya leo haina  watu wenye kiu ya kusoma vitabu,’’ amesema Bw. Buchafwe.

Amewaomba wazazi na viongozi katika taasisi za elimu kuwatiamoyo na kuwahimiza vijana kusoma vitabu, na kueleza kwamba kwa tabia watu wenye elimu na maarifa ya kisasa ni watu wanasoma sana na watu wasiosoma wana maarifa kidogo ya kileo.

“Kitabu hiki mbali ya kuangazia mambo ya kiimani lakini pia kimeangazia mambo ya biashara, siasa, uchumi na upendo ambayo yamekuwa muhimu katika kuchochea maendeleo ya mtu binafsi na Taifa kwa ujumla,’’ ameeleza Bw. Buchafwe na kusema kwamba angefurahi kupokea mrejesho wasomaji wa imani zote.

Bw. Buchafwe amesema kuwa imemchukua takribani miaka 16 kuandaa  na kupata mchapishaji  ambaye ameyaunganisha mashairi  na kuwa kitabu cha kurasa 84.
“Haikuwa kazi rahisi kukamilisha kitabu hiki, changamoto zilikuwa nyingi lakini nilizitumia katika kujenga maudhui yaliyobora zaidi kwa faida ya wasomaji,’’ amesema.

Bw. Buchafwe ana  Shahada ya Uzamili ya Mahusiano kwa Umma kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustiono (SAUT).  Ametafasiri vitabu viwili katika lugha ya Kiswahili  kutoka lugha ya Kingereza: Think Big  na God Sent a Man.

Comments

Popular posts from this blog

Kirenga: Kipaumbele chetu ni mkulima mdogo kupata soko la uhakika

NEMC warns on emptying effluent in built-up areas, flood waters

Gold mine in Songwe wins ministerial praise for protecting environment