Kampuni ya TCCIA Investment yapata faida ya milioni 366.57 mwaka 2018


Na Abdalah Luambano, Dar es Salaam
KAMPUNI ya TCCIA Investment Plc imesema jijini Dar es Salaam kwamba imepata faida ya shillingi 366.57 milioni kati ya mwaka 2018 ikilinganishwa na  milioni 246.57 za mwaka 2017 and  milioni 154.17 za mwaka 2016.
“Kampuni yetu inaendelea vizuri”, Mwenyekiti wa Bodi ya kampuni hiyo, Bw Fortunatus M. Magambo, ameuambia Mkutano Mkuu wa Mwaka  ambao ulifanyika jijini hivi karibuni.
Aliuambia mkutano huo kwamba  katika mwaka ulioisha Desemba 2018, faida ya kampuni kabla ya kodi ilishuka kwa asilimia 44 hadi 195.78 million ikilinganishwa na faida ya 2017 na kutaja sababu za kushuka huko kuwa ni pamoja na kupanda kwa gharama katika manunuzi.
Kisha akawapa habari njema wajumbe kwa kusema kwamba faida baada ya kodi ilipanda kwa asilimia 49 kufikia  milioni  366.57 kutokana na bidii iliyofanywa kuchanganua  na kusimamia mapato yatokanayo uwekezaji katika hati funani za serikali  na pia gawio kutoka kwa makampuni ambako TCCIA Investment imewekeza.
Mkutano uliidhinisha malipo ya gawio la shilingi 2.54 kwa kila hisa kama ilivyokuwa mwaka 2017.
Aidha kampuni hiyo, imewekeza kwenye mashirika na taasisi mbalimbali za fedha ikiwemo NMB, CRDB, Dar es Salaam Commercial Bank (DCB), Viwanda vya Saruji vya TWIGA, SIMBA, Tanzania Breweries (TBL), Swiss Port, na Kiwanda cha Sigara (TCC).
Tangu kuanzishwa kwa kampuni hii mwaka 2005, imeweza kufanya vizuri katika uendeshaji wake kiasi cha kuweza kujenga imani kubwa kwa wanahisa wake hapa nchini.
Kampuni ya wanahisa ya TCCIA Investment  ni moja ya kampuni za wanahisa inayofanya vizuri na kuchangia harakati za kuondokana na umasikini miongoni mwa jamii.
Mwisho.

Comments

Popular posts from this blog

Tanzania praised for being keen on fertilisers going to farmers

Gold mine in Songwe wins ministerial praise for protecting environment

NEMC warns on emptying effluent in built-up areas, flood waters