UDOM, Shell Tanzania Semina kwa wahitimu vyuo vikuu yawavuta wengi



Na Mwandishi Wetu, Dodoma


WASHIRI kwenye warsha ya kuwaandaa vijana na maisha mara wamalizapo masomo yao ya shahada ili waweze kwenda sambamba na soko la ajira wameipongeza Shell Tanzania kwa udhamini kwani imewajengea uwezo mkubwa.


Mafunzo hayo yametolewa Chuo Kikuu Dodoma ambapo wajasiriamali na wasomi wa kada mbalimbali waliwasilisha mada ili kuwapa vijana msukumo wa kupambana na soko la ajira ndani na nje ya Tanzania.


Akizungumza wakati wa semina hiyo iliyofanyika mwishoni mwa juma Kaimu Rasi wa Ndaki ya Sayansi za Ardhi, Dkt. Godlisten Kombe aliwashukuru kampuni ya Shell Tanzania kwa namna inavyosaidia jamii katika Nyanja mbalimbali ikiwemo elimu.


“Tunawashukuru sana wenzetu wa Shell Tanzania kwa kujitoa kwao katika kusaidia jamii za watanzania, kwa kipekee kabisa ni kwa namna walivyoitikia mwaliko wetu ili pamoja nasi kuweza  kuandaa warsha hii hapa UDOM katika Ndaki ya Sayansi na Ardhi, “ alisema Dkt Kombe.


Aidha Dkt Kombe amesema kuwa mafunzo haya yamekuja katika wakati muafaka ili kuwajenga wanafunzi na hasa tunapoelekea uchumi wa kati na wa viwanda ifikapo 2025.


“Jitihada hizi zina maana kubwa sana kwetu kama Chuo na Taifa kwa ujumla kwa kuwa inawafanya vijana wawe na chachu ya kutafuta na kufanya kazi kwa bidii na hivyo kuifanya sera ya uchumi wa kati na viwanda viweze kufikiwa kwa urahisi.” Alisisitiza Dkt Kombe


Katika hatua nyingine Dkt Kombe alitumia nafasi hiyo kuto wito kwa taasisi na kampuni mbalimbali nchini zinajitokeza katika kuwasaidia watanzania katika nyanja mbalimbali kama ambavyo Shell Tanzania wanafanya.


“Nitoe wito kwaMakampuni mbalimbali kujitokeza katika kuwasaidia vijana katika kuwajengea uwezo na hatimae tukapata nguvu kazi ya kuzalisha katika sekta mbalimbali kama ambavyo Shell Tanzania wameguswa kwa vijana wa hapa Udom, ni matumaini yangu kuwa semina hii
itawabadilisha vijana.” Alisema Dkt Kombe


Kwa Upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Oxford Policy Management Tanzania (OPM), Dkt Charles Sokile aliwaasa vijana kutumia nafasi mbalimbali wanazozipata katika kujijengea uwezo ikiwemo semina hii iliyoandaliwa na Shell Tanzania kwa kuwa kuwa soko la ajira linaushindani mkubwa.
 “Vijana lazima wajifunze namna ya kujiongezea thamani itakayowafanya wapenye katika soko la ajira ambalo kwa sasa limekuwa na ushindani mkubwa, na njia mojawapo ni hii ambayo Shell wamewaonyesha lakini mbali na hii zipo nyingi huko mitaani, ni jukumu lao kuzitumia kwa
lengo la kufikia malengo yao ambayo wanakuwanayo wanapokuwa vyuoni,” alisema Dkt Sokile


Pia aliwataka vijana kutokuwa na aibu wakati wakiwa katika mwelekeo wa kutafuta mafanikio ambayo wamekuwa wakiyaota tangu wakiwa wadogo.


“Vijana wetu wamekuwa na changamoto nyingi katika soko la ajira lakini changamoto hizo baadhi zinatengenezwa na vijana wenyewe kwa kupuuza mambo ambayo wangekuwa na ujasiri wa kuyafanya wangefika mbali, hivyo lazima wawe na uthubutu,” alisema Dkt Sokile.


Simon Jackson ambaye ni Mwanafunzi wa mwaka wa tatu katika fani ya Uchenjuaji na uchakataji wa madini aliwashukuru kampuni ya Shell Tanzania kwa namna ambavyo waendaa semina hiyo kwani wao kama walengwa imewaongezea thamani kubwa.


“Tunawashukuru Shell Tanzani kwa kuwa semina hii imekuwa muhimu sana kwetu kwa kutuongezea thamani lakini muhimu zaidi ni kwa namna ilivyokutanisha wadau mbalimbali kutoka sekta tofauti,” alisema Bwana Jackson na kutoa wito kwa kampuni na taasisi zingine kuiga mfano wa Shell Tanzania.


Afisa Utafiti na Uzalishaji kutoka Shell Tanzania, Bw. Marcus Luoga alieleza kufurahishwa kwake na mwaliko wa Chuo  Kikuu Dodoma (UDOM) na Shell Tanzania walitumia nafasi hiyo kuwaleta wataalam mbalimbali kwa lengo la kueleza vijana njia za kupita ili kufikia malengo yao.


“Tunaushukuru uongozi wa Chuo Kikuu Dodoma hususani ndaki ya sayansi za ardhi kwa namna walivyoona mchango wa Shell Tanzania na hivyo kutualika katika tukio hili muhimu. Shell Tanzania tumewaalika wataalamu mbalimbali ili kuelezea namna nzuri inayoweza kuwasaidia wahitimu wa vyuo vikuu kufikia malengo yao.” Alisema bwana Luoga


Kampuni ya Shell inafanya kazi katika mataifa matano ambayo ni Uingereza,  Australia, Malasia, Marekani na Tanzania ambapo imekuwa ikitoa michango mbalimbali kwa jamii ili kuondokana na changamoto za maisha.


MWISHO.

Comments

Popular posts from this blog

Mbeya agro-processors get 5 acres to build 50 industries

Tanzania praised for being keen on fertilisers going to farmers

Majaliwa aipongeza kampuni ya zana za kilimo ya Agricom