Waziri Bashe azindua kiwanda cha pamba cha Chato
NAIBU Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe amezidua Kiwanda cha
Pamba cha Chato (CCU) na kuielezea hatua
kama mpango kabambe wa serikali ya Awamu
ya Tano chini ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli wa kujenga
sekta ya kilimo inayojitegemea sambamba na
uhakika wa upatikanaji wa malighafi.
Akizungumza mara baada ya kukizinduzi wa Kiwanda cha Pamba
cha Chato (CCU) mwishoni mwa wiki, Waziri
Bashe alisema kufufuliwa kwa kiwanda hicho mwanzo mzuri kwa wakulima pamba kuongoza uzalishaji na kuinua
vipato vyao.
“Mradi wa kufufua kiwanda hiki umegharimu jumla ya
shilingi
6,714,804,447 kutoka katika benki ya Maendeleo
ya Kilimo Tanzania (TADB) lengo
likiwa kuimarisha sekta ya kilimo ili kuwanufaisha wakulima wa pamba,’’ alisema Bw.Bashe huku
akishangiliwa.
Alisema kufufuliwa kwa kiwanda hicho ambacho kilisimama
kufanya
uzalishaji kwa miaka kadhaa kutawafanya wakulima
wilayani Chato na maeneo mengine
ya jirani kuongeza uzalishaji na hivyo kuleta unafuu wa maisha kwa wakulima.
“Serikali imedhamiria kuifanya sekta ya kilimo inajitegemea
kwa kuwa
mbali ya kutoa ajira kwa watanzania walio wengi
lakini pia imekuwa na mchango wa
asilimia 25 katika pato la Taifa,’’ alisema.
Aidha, waziri Bashe aliipongeza Benki ya Kilimo kwa
jitihada zake za kuwaletea wakulima maendeleo kwa
kuwapa mikopo yenye mashrti nafuu jambo
ambalo linaongeza tija katika ukuaji wa uchumi wa Nchi.
“Natoa pongezi kwa TADB, Wizara, wadau wa kilimo pamoja na
chama cha ushirika wilayani chato (CCU)
kwa namna tulivyoshirikiana kuhakikisha kiwanda hiki kinaendelea na uzalishaji na hivyo kuchochea uzalishaji
wa zao la pamba,’’ alisema na kuziomba taasisi
zingine za fedha
kujitokeza na kuwekeza katika sekta ya kilimo.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Japhet Justine
alisema
kuzinduliwa kwa kiwanda hicho kutaongeza thamani
ya zao la pamba ambayo ilishuka
tangu msimu wa 2013/14.
“Tunaamini hatua tunazochukua kwa mazao ya kimkakati ikiwemo
zao la
pamba iyasaidia katika kuongeza thamani yake na
hivyo kuwa na bei ambayo itamfanya
mkulima anufaike zaidi na kuchungia ukuaji wa pato la Taifa,’’ alisema.
Alisema bei ya msimu huu imekuwa nzuri ukilinganisha na
misimu kadhaa ya hapo awali na kwamba
wataendelea kuimarisha upatikanaji wa soko zuri na lenye faida kwa mkulima.
“Msimu unaomalizika tulijitahidi kununua pamba kwa wakulima
kwa bei
ambayo waliifurahia lakini tunaendelea kuweka
mikakati ya kulifanya zao la pamba
kuwa na faida zaidi kwa kufufua viwanda vya kuchakata pamba kama hiki cha Chato,’’ alisema Bashe.
Naye Mmoja wa viongozi wa Chama cha Msingi wilayani
humo ambaye jinalake alikupatikana mara moja , mbali ya kuishukuru benki
ya kilimo alisema kufufuliwa kwa kiwanda
hicho kutaongeza ajira kwa watanzania.
“Kufufuliwa kwa kiwanda hiki kutaleta manufaa makubwa kwa
wananchi wa Chato kwani wataongeza kipato
chao na kumudu gharama za maisha na pia kuongeza ajira za moja kwa moja kiwandani,’’ alisema.
Kiwanda hicho kitanufaisha Vyama vya Ushirika wa kilimo na
Masoko
(AMCOS) 52 vyenye jumla ya wakulima 7000 kutoka
Chato, Biharamulo na Muleba.
Comments
Post a Comment