Posts

Showing posts with the label Main News

Mkutano mkuu TPSF kutathmini muundo, utendaji wake

Mkutano  mkuu TPSF  kutathmini  muundo, utendaji wake Daniel Lwimiko, Dar es salaam MAANDALIZI ya Mkutano  Mkuu wa  19 wa Mwaka (AGM) wa Taasisi ya Sekta Binafsi nchini (TPSF) unaotarajiwa kufanyika Jijini Dar es Salaam kesho yamekamilika ambapo wanachama wameombwa kushiriki kwa wingi pamoja nakufanya tathmini ya utendaji  na kuangalia muundo wake ili kuendana na wakati. Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo, Bw. Godfrey Simbeye alisema wajumbe watapata nafasi kujadiliana masuala mbalimbali ikiwemo muundo wa taasisi ili kukidhi matarajio ya wadau wote katika sekta za biashara na uchumi. “Mkutao huo wa siku moja umelenga kupitia upya muundo wa TPSF na namna ya kuwafikia wanachama wapya ili kwenda sambamba na azma ya serikali ya Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli ya kujenga uchumi wa kati na viwanda ifikapo mwaka 2025,” alisema Bw. Simbeye. Alisema TPSF kama taasisi inayosimamia

Kigamboni gets world class secondary school

Image
By our Correspondent, Kigamboni A private world class boarding secondary school has been established in Kigamboni District, one of Dar es Salaam Region’s new districts. The Director of Ihsan Islamic Secondary School, Dr  Hashim Saiboko,  told journalists who visited the school here yesterday that the school has been established in a bid to contribute to the government’s  turn round endeavours that seek to give Tanzanian pupils world class quality education. He said the Ministry of Education, Science, Technology and Vocational   Training, is playing its part, adding that it is important for school managements play a very supportive role to the government so that Tanzania can have citizens with world class education. Dr  Saiboko said “We have invested heavily in this school.  The primary aim for starting this school is to address professionally and eliminate the gaps in the current syllabus to allow Tanzanians pupils and students access world class quality education.” The

Kirenga: Safari kuelekea Tanzania ya viwanda inadai ufanisi

Image
Na David  Nawepa, Mbeya Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Kuendeleza Kilimo Kusini mwa Tanzania (SAGCOT), Bwana Geoffrey Kirenga, amesema Jijini hapa leo (Agosti 8, 2017) katika hafla ya kufunga maonyesho ya Nane Nane kwamba safari ya kuelekea Tanzania ya uchumi wa viwanda inadai utendaji wenye ufanisi katika maeneo yote ya sekta ya kilimo. “Tunapokwenda kwenye Tanzanaia ya viwanda lazima huduma hizi zitolewe kwa ufanisi zaidi,” amesema Bw. Kirenga, ambaye shirika lake limezoa sifa tele na kuvutia watu wengi kwa kuwa lilikuwa na mabanda zaidi ya 30 ya mashirika ya umma na binafsi katika eneo lilojulikana kwa jina la Sagcot Square.  Katika  Sagcot Square  washiriki walionyesha kwamba ubia kati ya sekta ya umma na sekta binafsi unawezekana na pia kuonyesha kwamba ubia huo una maslahi makubwa kwa taifa inapokuwa sekta hizi zinafanyakazi kwa karibu sana na kwa kuaminiana. Kadhalika Bw. Kirenga amepigania taasisi au mashirika yanayojihusisha na kilimo kwa kueleza kwamba yanahita