Sagcot Kichocheo yapongezwa kwa kuinua wakulima wadogo
NAIBU Waziri wa Kilimo Innocent Bashungwa akielezea jambo alipotembele makao makuu ya Mfuko wa SAGCOT Kichocheo yaliyopo jijini Dar es Salaam ikiwa ni ziara yake ya kwanza toka ateuliwe na Rais wa jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe, Dkt. John Pombe Magufuli.
NAIBU Waziri wa Kilimo Innocent Bashungwa akizungumza jambo na watendaji wa Mfuko wa SAGCOT Kichocheo(Sagcot Catalytic Trust Fund [CTF]) alipotembelea makao makuu ya ofisi hizo jijini Dar es Salaam ikiwa ni ziara yake ya kwanza toka ateuliwe na Rais wa jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe, Dkt. John Pombe Magufuli.
Na Abdallah Luambano, Dar es Salaam
SAGCOT Kichocheo (Sagcot Catalytic Trust Fund [CTF]) imepongezwa
na Naibu Waziri wa Kilimo, Bw. Innocent Bashungwa,kwa kuwainua wakulima wadogo
na kuwaingiza katika kilimo chenye tija.
Ameiambia hafla katika ofisi za mfuko huo baada
ya kutembelea taasisi hiyo Jijini Dar es Salaam kwamba kilimo chenye
tija kitachagiza maendeleo ya haraka kwa Taifa.
Bw. Bashungwa amesema Serikali imejipanga kuhahikisha wakulima
wanapata pembejeo kwa wakati, kuwapa mitaji na kutafuta masoko kwa mazao yote
ya kimkakati ili kufikia adhima ya serikali ya kutokomeza umasikini
unaowakabili wakulima na Taifa kwa ujumla
“Serikali inafanya jitihada kubwa katika kumtafutia mkulima
masoko ya mazao yake, kuagiza pembejeo nje ya nchi ili mkulima azipate kwa bei
nafuu pamoja na kuwapa mitaji kupitia taasisi zake mbalimbali ,” amesema Bw.
Bashungwa, na kuongeza kwamba Serikali imejipanga kuhahikisha wakulima wanapata
pembejeo kwa wakati, mitaji na masoko.
Ametoa ameushauri mfuko kushirikiana na taasis nyingine
zinazojihusisha moja kwa moja na kilimoi kubuni mpango endelevu wa kumsaidia
mkulima kushinda umaskini. Ametaja taasisi za aina hiyo kuwa ni
Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB).
“Nichukue nafasi hii kuwapongeza kwa kazi kubwa mnazozifanya
licha ya changamoto kadhaa mlizonieleza. Kwa ushirikiano wenu na
wadau wa sekta hii na mipango iliyopo tutafikia malengo ya
Serikali ya kufikia uchumi wa kati kwa kujenga viwanda. Tukumbuke kuwa kilimo
kinaajiri zaidi ya asilimia 65 ya Watanzania na ni chanzo
kikubwa cha malighafi,” amesema Naibu Waziri huyo.
Katibu Mtendaji wa mfuko huwo, Bw. John Kyaruzi, amemshukuru
Naibu Waziri kwa ziara yake na kueleza kwamba imetoa fursa kwa mfuko kueleza
mafanikio na changamoto ambazo wanakutananazo katika kutimiza
malengo yake.
“Hii ni fursa adhimu kutembelewa na Naibu Waziri, tunashukuru
sana na tumetumia nafasi hii kueleza mambo tunayokabiliana nayo katika
utekelezaji wa majukumu yetu.” Alisema Bw. Kyaruzi
Bw. Kyaruzi alimhakikishia Waziri kuwa taasisi yake itayafanyia
kazi mapendekezo yote kwani kimsingi yatamsaidia mkulima kutokana na umasikini
kwa kuenzi kilimo chenye tija.
Tangu kuanzishwa kwa mfuko umejenga maghala katika maeneo
mbalimbali katika mikoa ya nyanda za juu kusini, umetoa wa mikopo yenye
masharti nafuu, kusambaza pembejeo na kwa wakulima
wadogo.
Mwisho.
Comments
Post a Comment